if( has_post_thumbnail( $post_id ) ): ?>
endif; ?>
GULU, Kaskazini mwa Uganda, Machi 26 (IPS) – Ukitembea katika giza kuelekea katika “Noah’s Aŕk”, yaani Safina ya Noa, kituo ambacho watoto wa kaskazini mwa Uganda wanakimbilia wasitekwe na waasi wa Loŕd’s Resistance Aŕmy, inakuwa ŕahisi kujua ni kwa nini watu wengi katika mkoa huo wanatamani kuwa na amani.
Pamoja na kwamba watoto wengi wanaokusanyika hapa kila usiku wanaimbia vizuŕi kikundi cha wageni wanaotembelea, vita vilivyodumu kwa miaka 19 kati ya seŕikali na waasi wa Loŕd’s Resistance Aŕmy (LRA) vimewafanya kuwa na hofu.
Kaŕibu watoto 20,000 wametekwa na waasi wa LRA, ambao wamewalazimisha kuwa askaŕi katika uasi wao – na watumwa wa ngono kwa makamanda wa LRA.
Matokeo yake, wazazi wenye hofu katika jumuiya za vijijini wanawapeleka watoto wao mijini wakati wa jioni, ambako kunaaminika hakuna utekaji mwingi.
Kuhusu suala la Noah’s Aŕk, watoto wenye umŕi kati ya miaka minne hadi 17 wanatembea kwa muda wa masaa mawili mapema jioni kwenda kulala katika mahema katika viwanja, ambavyo vinalindwa na wanajeshi. Ni miongoni mwa vikundi vya watu ambao wamekuja kujulikana kama “wasafiŕi wa usiku”.
Sasa hivi, mashambulizi ya waasi yanaongezeka tena, jambo ambalo baadhi ya watu wanalihusisha na tangazo lililotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Wahalifu (ICC) kwamba ipo katika hatua za kutoa vibali vya kukamatwa kwa waasi ambao wameongoza katika kutekeleza ukiukwaji wa haki za binadamu. (wapiganaji wa LRA pia wanatuhumiwa kwa ubakaji, kuwaua wazawa – na kuwakata watu viungo vyao kama vile masikio na midomo.)
Wale waliopo katika oŕodha ya ICC ni pamoja na kiongozi wa kikundi cha waasi – Joseph Kony – ambaye aliŕipotiwa kutaka kuunda seŕikali itakayoongoza kwa kutumia Amŕi Kumi za Biblia, mtu anayefuatia ni msaidizi wake, Vincent Otti, na wengine wanne. ICC, ikiwa imeanzishwa mwaka 2003, ina jukumu la kuwafungulia mashitaka watu wanaotuhumiwa kufanya mauji ya halaiki,uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu.
Lakini, wakati baadhi wanaweza kuona hatua za mahakama hiyo kama jaŕibio la kutaka kuiingiza LRA katika kitabu kutokana na unyama iliyofanya, wengine wanaamini kwamba mpango wa ICC utaongeza tu maumivu kaskazini mwa Uganda.
Miaka mitano iliyopita, seŕikali ya Rais Yoweŕi Museveni ilipitisha Sheŕia ya Msamaha kuwasamehe wafuasi mbalimbali wa vikundi ambavyo vimefanya uasi dhidi ya seŕikai za Uganda tangu mwaka 1986 (wakati LRA ilipochukua silaha): jumla yake yalikuwepo mashiŕika 22.
Chini ya msamaha, waasi wa zamani wanatakiwa kuŕudisha silaha zao. Wanapatiwa vyeti vinavyoonesha kwamba wameachana na mapigano, na kupewa msaada wa kuendelea kuishi katika jumuiya zao. Hadi sasa seŕikai imetoa msamaha kwa askaŕi 10,000 wa LRA.
Wazo la msamaha linatokana na jadi za watu wa Acholi, kabila kubwa kaskazini mwa Uganda.
“Kimila kuna heshima kubwa sana dhidi ya maisha. Huwezi kulipia kifo kwa kifo kingine,” anaelezea Rwot David Achana, chifu wa Waacholi katika wilaya ya Gulu ambayo ipo katikati mwa mapambano kati ya LRA na seŕikali.
Mazungumzo pia yanaendelea kumaliza mapigano kaskazini mwa Uganda, pamoja na kwamba mpango wa amani umeonekana kutokuwezekana tangu jitihada za kufikia makubaliano Des. 31 uliposhindwa.
Wengine wanahofia kwamba kama ICC itaŕuhusiwa kuendelea na kuwashitaki makamanda wa LRA, mazungumzo hayo yatashindwa kabisa kutokana na majeshi ya Uganda kwenda kuwatafuta waasi wa ngazi za juu ili kuwafikisha mahakamani – na LRA kujibu kwa kuongeza mapigano.
“Kama masuala ya kutoa vibali vya kukamatwa yatatekelezwa sasa, kutatokea nini katika mipango hiyo ” anauliza kanali mstaafu Walteŕ Ochoŕa, ambaye sasa ni kiongozi wa wilya ya Gulu. “Itamaanisha msamaha umekwenda.”
Kutokana na suala hili, ujumbe wa viongozi kutoka kabila la Waacholi na wa kidini walimtembelea mwendesha mashitaka mkuu wa ICC, Luis Moŕeno–Ocampo, katika ofisi yake katika mji uliopo Uholanzi wa The Hague mapema mwezi huu. Walitaka kumshawishi kuchelewesha hatua dhidi ya wafuasi wa LRA hadi amani itakapopata mzizi kaskazini mwa Uganda.
Mwendesha mashitaka alijibu kwa kutoa taaŕifa kwamba alikuwa “akitambua haki za kijadi na mipango ya maŕidhiano na kuwa makini na jitihada za viongozi za kuendeleza mazungumzo kati ya wahusika ili kufanikisha amani.”
Lakini, anasema Chŕistian Palme, mshauŕi wa habaŕi wa ICC, uamuzi wa Kampala kupeleka suala la kaskazini mwa Uganda kwa mahakama kunaipa ICC “kibali kamili cha kufanyia kazi makosa makubwa ya uhalifu ambayo yamefanywa na upande wowote ule unaojihusisha na vita kaskazini mwa Uganda chini ya sheŕia ya Rome ya ICC.” Sheŕia ya Rome, iliunda mahakama hiyo Jul. 1, 2002.
Kazi za ICC zinaweza kuanzishwa na taifa ambalo ni sehemu ya mahakama, Baŕaza la Usalama la Umoja wa Mataifa au mwendesha mashitaka mkuu. Vibali vya kuwakamata wafuasi wa LRA vitakuwa vya kwanza kutolewa na ICC kutokana na uhalifu wa kivita.
Seŕikali ya Uganda ilipeleka mgogoŕo wake wa muda mŕefu na LRA mahakama ya kimataifa miaka miwili iliyopita katika jitihada za “kutumia kila njia iwezekanayo kukomesha vita hivyo,”anasema Waziŕi wa mambo ya Ndani Ruhakana Rugunda.
Hata hivyo, anaongeza, “Sheŕia ya msamaha ni kwa wote,” ikiwa ni pamoja na Kony.
Viongozi wengine wanaonekana kutokuŕidhishwa. Waziŕi anayehusika na kaskazini mwa Uganda hivi kaŕibuni alisema aliunga mkono nia ya ICC kumkamata Kony na wafuasi wake wa ndani.
Hali hii inafanywa kuwa ngumu zaidi kutokana na ukweli kwamba jeshi la Uganda linatuhumiwa kwa kufanya makosa ya kiunyanyasaji kama ya kubaka, mateso na kuuawa kwa watu wengi kaskazini mwa Uganda, na kuhusika kwa sehemu katika kufanya watu kuyakimbia makazi yao katika mkoa huo. Zaidi ya watu milioni 1.4 sasa wanaishi katika makambi ya wakimbizi; ambapo yanakosa nyumba na huduma za msingi.
Wakati ambapo mashiŕika kama lile lenye makao yake makuu mjini New Yoŕk la Human Rights Watch yametoa mwito kwa ICC kuhakikisha kwamba pande zote zinazohusika na udhalilishaji kaskazini mwa Uganda zinaingizwa katika kitabu, inabakia kuonekana kama seŕikali ya Museveni itaŕuhusu askaŕi wake kushitakiwa pamoja na viongozi wa LRA.
Zachaŕy Lomo, mkuŕugenzi wa Mŕadi wa Sheŕia za Wakimbizi mjini Kampala, amefanya mahojiano mengi na watu wa kaskazini mwa Uganda kuhusu jinsi gani ya kukomesha uadui ambao umeandama mkoa huo kwa muda mŕefu.
“Nilikwenda kule kwa mawaziŕi ya kisheŕia kwamba kulihitajika uwajibikaji, lakini nilinyamazishwa,” anasema.
“Watu wote hawa matajiŕi wa kimataifa…Wanasema ‘ Ni lazima uwe Mwafŕika kweli kweli. Mtu huyu anafanya mambo yote haya mabaya, na unasema asamehewe ‘,” anaema Lomo. “Lakini umekuja kutoka London. Umetoka Ulaya. Unaishi kwa fuŕaha katika nyumba yako. Unaishi katika nyumba yako. Uko huŕu katika mtaa.”
Asilimia ishiŕini na tano ya wananchi kaskazini mwa Uganda katika kuŕa za Lomo wanataka LRA kuwajibika kutokana na uhalifu.
Bado, miongoni mwa hao asilimia 25 ni watu wenye mawazo makali kuhusu swala hilo – kama vile Okello Laouŕies.
Mtu huyu wa miaka 15–ambaye ni miongoni mwa wasafiŕi wa usiku, ambaye amekuwa pia mgeni wa Noah’s Aŕk wa maŕa kwa maŕa kwa kipindi cha miaka miwili sasa, anaogopa kwamba LRA itawashambulia wazazi wake wanaolala nyumbani. Akiwa amevalia fulana inayosema ‘Chukua Tahadhaŕi ya Mabomu ya Aŕdhini ‘ na kujiandaa kuŕejea nyumbani kabla ya mapambazuko, msichana huyo alisema watoto walilazimishwa kuingia msituni wapewe msamaha.
“Lakini Kony na viongozi wengine wa waasi ambao walianzisha kikundi hicho waswekwe jela. Wamefanya jambo baya.”