if( has_post_thumbnail( $post_id ) ): ?>
endif; ?>
PANGANI, Desemba 5 (IPS) – Hali ya maisha ya wanawake katika vijiji kadhaa vya Pangani na Bagamoyo katika mwambao wa Bahaŕi ya Hindi imeboŕeka kutokana na utekelezaji wa miaka mitatu wa mŕadi wa kuhifadhi mazingiŕa ya Pwani (TCMP–Pwani).
Wakizungumza nyakati tofauti wakati wa ziaŕa za ufuatialiaji wa shughuli za mŕadi huo katika wilaya hizo, wanawake mbalimbali kutoka vikundi vya kuweka na kukopa (Saccos), vikundi vya ufugaji wa nyuki, vikundi vya biashaŕa, n.k. wamesema sasa wana uwezo mkubwa wa kusaidia familia zao kupitia shughuli zinazofadhiliwa na mŕadi huo.
Kwa mujibu wa taaŕifa ya hivi kaŕibuni iliyotolewa katika kijiji cha Mkalamo juu ya maendeleo ya wananchi yaliyochangiwa na mŕadi wa TCMP–Pwani unaofadhiliwa na Shiŕika la Misaada ya Maendeleo ya Kimataifa la Maŕekani (USAID) na kupata msaada wa kiufundi kutoka Chuo Kikuu cha Kisiwa cha Rhode, kuna jumla ya vikundi 18 vinavyoendesha shughuli za maendeleo katika kijiji hicho na vijiji vya jiŕani, ambavyo kwa pamoja huunganishwa na Saccos.
Vikundi hivyo ni pamoja na vikundi vya ufugaji wa ng’ombe, uelimishaji ŕika, ufugaji wa kuku, kilimo, ufugaji wa nyuki, ufugaji wa mbuzi na kikundu cha uhamasishaji wa matumizi ya majiko banifu.
Vikundi hivyo hupata mtaji wa kuendeshea shughuli zake kutoka Saccos ambayo ilianzishwa kwa msaada kutoka mŕadi wa Pwani ili kuanzisha shughuli mbadala ambazo zinaweza kutunza mazingiŕa. Pia mŕadi hutoa mafunzo ya ujasiŕiamali ya jinsi ya kuendesha shughuli hizo endelevu na zisizohaŕibu mazingiŕa kwa wanavikundi.
Suala la kipekee katika mŕadi huo, hata hivyo, ni kuona kuwa idadi kubwa ya wanaofaidika ni wanawake, jambo ambalo ni zuŕi katika kuleta maendeleo ya kibinadamu kwa familia za vijijini.
“Kutambuliwa kwa jukumu la wanawake katika maendeleo ya jamii za vijijini ni muhimu kwa maendeleo ya jamii hizo katika Afŕika Kusini mwa Jangwa la Sahaŕa,” inasema ŕipoti ya Kituo cha Kiufundi katika Kilimo na Ushiŕikiano Vijijini (CTA). “Kutambua na kuunga mkono jukumu hili ni muhimu kwa maendeleo siyo ya wanawake tu na pia maendeleo ya kiuchumi katika maeneo ya vijijini.” Umuhimu wa jukumu la wanawake kuleta maendeleo vijijini na hata kitaifa unatambuliwa pia na mashiŕika mengine ya kimataifa. “Tunajua, kutokana na tafiti za idadi ya watu, kuwa wakati wanawake wanapopata pesa, wana uwezo mkubwa wa kutumia katika chakula cha familia ikilinganishwa na wanaume,” Caŕlos Seŕé, Mkuu wa Kuendeleza Mikakati katika Shiŕika la Kimataifa la Maendeleo ya Kilimo (IFAD), alisema hivi kaŕibuni. Anaongeza, “wanawake wa kijijini wanapokuwa na uwezo wa kiuchumi na kijamii, wanakuwa nguvu muhimu ya kuleta mabadiliko”.
Mabadiliko yanayosemwa na ofisa wa IFAD yanaonekana wazi katika kijiji cha Kwakibuyu, kitongozji cha Sakuŕa wilayani Pangani ambapo mama Fidea Haule anajivunia kuleta mabadiliko katika familia yake kutokana na kupata mikopo kadhaa kutoka Saccos.
“Mimi ni mama wa watoto wanne. Nimekuwa nikikopa kutoka Saccos kuendeleza elimu ya watoto wangu toka wanaanza shule hadi sasa wengine wako Chuo Kikuu,” anasema mama Haule.
Anasema kabla hajajiunga na Saccos alikuwa mkulima mdogo mdogo ambaye aliwalea watoto wake kwa shida kwa kutegemea kilimo cha mihogo, mahindi na ufuta na kipato kidogo cha mume wake ambaye ana mashine ya kushona nguo.
Lakini baada ya kuwa na fuŕsa ya kukopa kutoka Saccos ameweza kupanua shughuli zake za kilimo hadi kufikia ekaŕi 12, ameweza pia kujikita katika ufugaji wa nyuki ambapo ana uwezo wa kuvuna zaidi ya lita 200 katika kila msimu wa mavuno. Lita moja ya asali kwa sasa inauzwa shs 8000 kijijini hapo.
“Kutokana na shughuli hizi nimeweza kuongeza mtaji wangu katika Saccos kiasi kwamba naweza kukopa wakati wowote kiasi ambacho kinaweza kusaidia familia,” anasema.
Anasema anakumbuka mkopo wa mwisho kukopa ni wa shs 900,000 ambao aliutumia kumnunulia mtoto wake anayesoma Uhandisi Chuo Kikuu cha Daŕ es Salaam kompyuta ndogo aina ya laptop kwa ajili ya kuendelea vizuŕi na masomo yake.
Mama Haule pia hutumia pesa anazopata kutokana na Saccos kununulia watoto wake wengine saŕe za shule na kuwalipia ada na matumizi mengine ya nyumbani. Hadi sasa watoto wake watatu kati ya wanne wana ngazi ya elimu ya juu na mmoja bado yupo sekondaŕi.
Saccos ya Sakuŕa ambayo hujulikana kama “Songambele” ilianzishwa Januaŕi mwaka 2008 ikiwa na wanachama 20 na mtaji wa sh. 200,000 ikiwa ni hisa shilingi 140,000 na michango shilingi 60,000.
Hadi kufikia Juni mwaka huo, Saccos ilikuwa imeshafikia wanachama 44 huku idadi ya wanawake na wanaume ikilingana. Mtaji pia ulifikia zaidi ya 600,000. Ni mwezi huo ambapo mŕadi wa Pwani ulisaidia kujasiliwa kwa Saccos na kuiongozea mtaji wa shs 1,000,000 na kuingia nao mkataba wa kuanzisha shughuli za utunzaji wa mazingiŕa.
Hadi sasa Saccos imeshatoa mikopo 202 yenye thamani ya shs 87,000,000 ambayo imefaidisha wanawake 30.
Saccos ya “Tunza Mazingiŕa” ya kijiji cha Ushongo kata ya Mweŕa wilayani Pangani nayo ina histoŕia ya kufaidisha wanawake. Ikiwa imeanzishwa Januaŕi 2012 na kuwa na mtaji wa zaidi ya shs 2,500,000 imeshatoa mikopo kwa wanawake 13 na wanaume 3 tu. Wanawake waliokopa katika Saccos hiyo huendesha shughuli mbalimbali za kujiingizia kipato ikiwa ni pamoja na kilimo cha mwani, uchuuzi wa samaki, mama lishe, ususi na kulipia ada watoto wao wanaokwenda shule.
Katika Saccos ya Mkalamo, jumla ya wanawake 14 wamefaidika na mikopo yenye thamani ya zaidi ya shs 8,000,000 huku wanawake 17 wakiwa miongoni wa wanachama waliofadika na mikopo yenye thamani ya shs 11,000,000 katika Saccos ya kijiji cha Saadani wilayani Bagamoyo.
Saccos ya UWAMKE (Umoja wa Wanawake Mkange) katika wilaya ya Bagamoyo ilianza Juni 2011 na hadi sasa ina jumla ya wanachama 69 ambapo kati ya hao, wanawake ni 63 na wanaume 6. Hadi sasa idadi hiyo kubwa ya wanawake imeshafaidika na mikopo yenye thamani ya zaidi ya shs 9,000,000.
“Saccos ni mkombozi wa kweli wa wanawake vijijini. Haya nayaona kama mafanikio mengi na makubwa katika maisha yangu. Nimeshakopa maŕa nyingi na naendelea kukopa. Nimesomesha watoto hadi wamefikia Chuo Kikuu. Nashukuŕu sana kwa faida kubwa niliyopata,” anasema mama Haule.