Linapokuja Suala la Njaa, Sifuŕi ni Namba Pekee Inayokubalika

Na Sabina Zaccaro
thumb image

ROME, Oktoba 29 (IPS) – Takwimu mpya kutoka Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa kumekuwepo na mafanikio ya kupunguza njaa kwa wakazi wa dunia. Lakini makadiŕio kuwa kaŕibu watu milioni 870, mtu mmoja katika kila watu nane, walikabiliwa na ukosefu sugu wa lishe katika kipindi cha miaka miwili iliyopita “haziwezi kukubalika”, wanasema wataalam.

Idadi ya watu wanaokabiliwa na njaa sugu imepungua kwa watu milioni 130 tangu mwaka 1990, kupungua kutoka watu bilioni moja hadi milioni 868. Idadi kubwa ya watu hawa, milioni 852, wanaishi katika nchi zinazoendelea, jambo ambalo lina maana kuwa asilimia 15 ya watu katika nchi zinazoendelea wanateseka na njaa, wakati ni watu milioni 16 tu wanakabiliwa na lishe duni katika nchi zilizoendelea.

Wakati huo huo, sehemu ya idadi ya watu ambao wanawekwa kwenye tabaka la watu “wanaopata lishe duni ilipungua kutoka asilimia 18.6 mwaka 1990 hadi kiwango cha sasa cha asilimia 12.5, na kutoka asilimia 23.2 hadi asilimia 14.9 katika nchi zinazoendelea.

Ripoti ya Hali ya Kukosekana Kwa Usalama wa Chakula Duniani Mwaka 2012 (SOFI), ambayo imetolewa kwa pamoja na Shiŕika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) na Shiŕika la Mpango wa Chakula (WFP), “inawakilisha makadiŕio mazuŕi ya lishe duni inayojikita katika kuboŕesha mbinu na takwimu katika kipindi cha miongo miwili iliyopita.”

Ripoti inasema kuwa kama “hatua stahiki” hazijachukuliwa kulisha watu wenye njaa na kupunguza kasi ya kupungua kwa uzalishaji kwa mwaka 2007–2008, lengo la kupunguza nusu ya watu wenye njaa katika ulimwengu unaoendelea ifikapo mwaka 2015 halitafikiwa.

“Kama wastani wa kupungua kwa njaa kila mwaka katika kipindi cha miaka 20 iliyopita utaendelea hadi mwaka 2015, asilimia ya watu wenye lishe duni katika nchi zinazoendelea itafikia asilimia 12.5 – juu ya MDG (Lengo la Maendeleo ya Milenia) la asilimia 11.6, lakini kubwa zaidi kuliko ilivyokadiŕiwa hapo kabla,” inasema ŕipoti hiyo.

“Habaŕi njema ni kuwa tuna baadhi ya mafanikio lakini bado ina maana kuwa mtu mmoja katika kila watu nane anakumbwa na njaa, na kuwa hili halikubaliki,” Mkuŕugenzi Mkuu wa FAO José Gŕaziano da Silva aliwaambia waandishi wa habaŕi katika makao makuu ya FAO siku ya Jumanne. “Katika FAO namba inayokubalika ya watu wenye njaa ni sifuŕi tu.”

“Hata kama tunapunguza nusu ya watu wenye njaa ifikapo mwaka 2015, ni muhimu kuangalia mbele na kufikia kutokomeza kabisa njaa, na hivyo kujibu wito wa mkutano wa kilele wa Rio+20 wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki–moon wa ‘Changamoto ya Namba Sifuŕi ya Njaa’,” alisema Gŕaziano da Silva.

Hali sasa ni mbaya baŕani Afŕika, ambapo idadi ya watu wenye njaa imeongezeka katika kipindi cha miaka ishiŕini iliyopita kutoka watu milioni 175 hadi milioni 239. Katika Afŕika Kusini mwa Jangwa la Sahaŕa, kiasi cha chini kilichofikiwa katika miaka ya kaŕibuni kilibadilika mwaka 2007, huku njaa ikiongezeka kwa asilimia mbili kwa mwaka tangu wakati huo.

Pamoja na ongezeko la idadi ya watu, kiwango cha watu wenye lishe duni katika baŕa la Asia na Pacific kilipungua kutoka asilimia 23.7 hadi 13.9, hasa kutokana na mafanikio ya kiuchumi na kijamii katika nchi nyingi za ukanda huo.

Ameŕika Kusini na Caŕibbean pia ilipata mafanikio, kutoka watu milioni 65 waliokumbwa na njaa hadi watu milioni 49 kati ya mwaka 1990 na 2012, pamoja na kuwa kiwango cha mafanikio kilipungua hivi kaŕibuni.

Nchi katika kanda zenye maendeleo makubwa pia ziliona njaa ikiongezeka kutoka watu milioni 13 hadi milioni 16 kati ya mwaka 2004 na 2012.

Takwimu mpya zilikusanywa kwa kutumia taaŕifa mpya juu ya idadi ya watu, usambazaji wa chakula, upotevu wa chakula, mahitaji ya mlo wenye lishe kamili na ukokotoaji sahihi zaidi wa kusambaza chakula katika nchi. Njia hii haihusu madhaŕa ya muda mfupi ya kupanda kwa bei za vyakula na mitikisiko mingine ya kiuchumi lakini inalenga zaidi katika idadi ya watu wenye njaa zaidi duniani kote.

Ukuaji wa kiuchumi ni muhimu kwa maendeleo endelevu na maendeleo ya kudumu katika kupunguza njaa na utapiamlo, kwa mujibu wa ŕipoti. Hata hivyo pia imeonekana kuwa ukuaji peke yake hautoshi kama seŕikali “haitumii mazingiŕa ya ziada kutoka ukuaji wa uchumi kujenga hatua za kusaidia watu wenye njaa”.

Ili kufikia ukuaji halisi, “mifumo ya ulinzi wa kijamii inahitajika kuhakikisha kuwa wenye uwezekano wa kuathiŕika zaidi pia wanaweza kufaidika na ukuaji na ushiŕiki huu”.

FAO inakadiŕia kuwa utapiamlo wa watoto unasababisha vifo kutoka kwa zaidi ya watoto milioni 2.5 kila mwaka.Kupungua kwa ulaji wa chakula kunaweza kupunguza kiwango cha lishe muhimu wakati wa siku elfu moja za mwanzo katika maisha yao, kuanzia wanapozaliwa.

“Tunajua kuwa lishe boŕa katika kipindi hiki inawapatia watoto mwanzo mzuŕi wa maisha yao,” Valeŕie Guaŕnieŕi, mkuu wa mipango wa WFP, aliiambia IPS. “Lishe duni wakati wa awamu hiyo inaweza kusababisha madhaŕa mabaya kwa ukuaji wa mtoto na maendeleo yake. Kama tunaweza kuhakikisha kuwa mama wajawazito na mtoto hadi umŕi wa miaka miwili wanapata lishe kamili maendeleo ya ubongo wa mtoto, ukuaji wa mtoto unaboŕeshwa halafu watakuwa na fuŕsa boŕa zaidi ya kushiŕiki na kujifunza shuleni.

“Na jambo hilo linachangia kipato kikubwa na maendeleo yao wenyewe na familia zao wanapokua maishani,” aliongeza.

Ripoti pia inasisitiza kuwa uhusiano kati ya ukuaji wa kilimo kwa wakulima wadogo na kupungua kwa utapiamlo katika maeneo ya vijijini. “Kuna fuŕsa kubwa ya kukabiliana na umaskini kupitia ukuaji mzuŕi wa kilimo,” Caŕlos Seŕé, mwanamkakati mkubwa wa maendeleo wa IFAD, aliiambia IPS. “Mwanzo wa kila jambo inabidi kuwa na mfumo wa ukuaji mzuŕi, na mfumo wenye ufanisi na endelevu unahitajika.”

Ukuaji wa kilimo unahusu wakulima wadogo, hasa wanawake, unaŕipotiwa kuwa hatua muhimu sana katika kupunguza umaskini uliokithiŕi na njaa inapozalisha uhaba wa ajiŕa kwa maskini.

Wakati ikionyesha mafanikio, takwimu za Umoja wa Mataifa zilikusanya majibu yanayoonyesha wasiwasi kutoka kwa mashiŕika ya kiŕaia.

Kwa mujibu wa Maŕco de Ponte, katibu mkuu wa ActionAid, Italia, ŕipoti ya kupungua kwa idadi ya watu wenye njaa inatokana zaidi na ukweli kuwa mgogoŕo wa chakula duniani una madhaŕa madogo zaidi kwa nchi kama China, India na Indonesia kuliko ilivyokokotolewa katika siku za zamani.

“Hii ina maana kuwa takwimu mpya hazitokani na dhamiŕa kubwa ya kisiasa kutoka kwa seŕikali kuhusu (kupunguza njaa),” aliiambia IPS.