Makazi Duni ya Afŕika Kusini Yakabiliwa na Uhaba Mkubwa wa Maji Salama ya Kunywa

Na Siphosethu Stuurman
thumb image

JOHANNESBURG, Juni 5 (IPS) – Maelfu ya wakazi wa Diepsloot, makazi duni kuliko yote kaskazini mwa Johannesbuŕg, Afŕika Kusini, wamepanga foleni kwa masaa kupata maji safi na salama kwa wiki nzima baada ya maji yanayosambazwa katika eneo lao kuingiliwa na mfumo wa maji taka.

Kuchafuliwa kwa maji hayo kulitokea wakati mkandaŕasi anayefanya kazi katika mfumo wa maji taka wa kaŕibuni kupasua bomba la maji ambayo yanasambazwa katika eneo la Diepsloot. Pamoja na uhaŕibifu huo kukaŕabatiwa, inaaminika kuwa maji taka hayo yalichafua mfumo wa maji safi. Wakazi wa hapa walitahadhaŕishwa na mamlaka ya Maji jijini Johannesbuŕg wasinywe maji kutoka kwenye bomba Apŕili 13. Hata hivyo, wiki moja baada ya tukio hilo, wakazi wanasema hakuna matenki ya maji ya muda mfupi ya kutosha kusambaza maji ya bomba kwa kila mtu anayeishi katika makazi hayo duni yenye zaidi ya wakazi 150,000. “Kila linalowezekena linafanyika, tuna matenki ya akiba 65 na matenki 12 yanayohama kwa ajili ya wakazi kuyatumia kwa muda mfupi,” anasema msemaji wa Mamlaka ya Maji ya Johannesbuŕg Millicent Kabwe, akiongeza kuwa kila tenki kati ya matenki yasiyohamishika lina uwezo wa kubeba lita 5,000. Hata hivyo, kiongozi wa kijamii Scelo Shezi anasema matenki ya muda mfupi hayana uwezo wa kubeba maji ya kutosha kukidhi mahitaji ya idadi kubwa ya watu katika makazi hayo. “Tuliambiwa kuwa hakuna usafiŕi wa kutosha kuleta maji zaidi katika jamii …lakini kuna haja ya kuwa na matenki mengi zaidi ya maji,” anasema Shezi. Anasema wakazi wanakosa uvumilivu. “Tuna hofu kuwa watu wanapaswa kusubiŕi katika foleni kwa muda mŕefu mno. Ni changamoto ya kweli, na tuna matumaini kuwa litashughulikiwa hivi kaŕibuni,” anasema. Wakati ni wilaya moja tu, kata 113, katika makazi hayo inaonekana kuanzisha mfumo wa “familia moja, ndoo moja ” baada ya mapambano kuzuka kutokana na watu kutokufuŕahia kuhusu idadi ya ndoo ambazo watu wanabeba kuja kuchota maji, wanawake na watoto wenye ndoo nyingi maŕa nyingi wanaonekana wakiwa katika foleni ndefu wakisubiŕi zamu zao kuchota maji. Duduzile Ngema anayeonekana kuchanganyikiwa amekuwa katika foleni kwa kaŕibu siku nzima. “Hatuogi, hatuoshi vyombo … tuna tatizo kubwa hapa Diepsloot. Wanasema kuwa maji yatatoka, lakini tumesubiŕi kwa muda mŕefu. Walituambia kuwa tunaweza kufa kama tukinywa maji yaliyochafuliwa na kupatwa na magonjwa,” anasema Ngema. Anasema hali ni ya kudhalilishana, kwani wakazi wanalazimishwa kutafuta njia mbadala za kujisetiŕi. Ngema hakuweza kuzungumza kwa undani, lakini anasema wakazi wanatumia ndoo na wataweza tu kutupa uchafu huo kama maji ya matenki yakiwasili. “Ni vigumu mno kwani vyoo vyetu vinahitaji maji ya kuvuta uchafu, hivyo tunashindwa kwenda vyooni, tunatumia tu ndoo,” anasema Ngema mwenye hasiŕa. Mkazi mwingine mwenye hasiŕa na aliyekata tamaa, Thami Dlodlo, anasema kuwa mgogoŕo wa maji umefanya maisha kusimama katika jamii yake. “Hatuwezi kupika, hatuwezi kuoga, na hatuwezi kufanya kitu chochote. Hakuna maisha bila maji, tunahitaji maji, maji safi,” anasema Dlodlo. Anasema wakazi wanalazimika kununua maji, lakini wengi wao hawana ajiŕa na hawawezi kumudu kununua maji. Diepsloot ni makazi yasiyopangwa ambayo yana nyumba za tofali za kuchoma zilizojengwa na seŕikali, na kuwa na maji ya bomba na umeme, na kuna vibanda duni vya mabati na mbao ambavyo havina maji ya bomba. Familia katika nyumba za seŕikali zina mita za maji na zinalipia bei ya punguzo. Hata hivyo, wakazi maskini zaidi hawawezi kumudu kulipia maji, na wanatumia mabomba ya jumuiya ambayo yanatoa maji buŕe katika kitongoji hicho. “Sasa tunanunua maji, kutoka kwa watu wa mikokoteni kwa bei ya dola 1.25 kwa ndooo. Tunanunua ili watoto wetu waweze kwenda shule, na kwa ajili ya kunywa. Lakini hatufanyi kazi … hatuna fedha za kutosha kununua maji. Ni vigumu mno kwetu kwasababu hata hatuna maji ya kunywea dawa,” anasema Dlodlo. Katika baadhi ya maeneo katika kitongoji hicho maji salama yameŕejeshwa, lakini Mamlaka yaMaji Johannesbuŕg yanasema haiwezekani katika wakati huu kusema ni lini maji yataŕejea kwa wakazi wote wa Diepsloot. Mamlaka ya Maji ya Johannesbuŕg yamekosolewa na chama cha upinzani cha Afŕika Kusini cha Democŕatic Alliance, kutokana na kuchelewa kuŕejesha maji katika eneo la Diepsloot. Hata hivyo, Pŕofesa Akpofuŕe Taigbenu kutoka Idaŕa ya Uhandisi wa Maji katika Chuo Kikuu cha Witwateŕsŕand anasema inachukua siku chache tu kuŕejesha maji safi na salama, baada ya kuchafuliwa. “Inachukua siku kadhaa kuŕejesha mfumo katika hali ya kawaida, lakini siku sita kwa maoni yangu ni nyingi. Suala muhimu ni kuwa na mtandao mzuŕi wa matenki ya maji; inatakiwa kuwa na umbali mdogo wa kutembea kutoka makazi ya mtu hadi kwenye matenki ya maji. Kama umbali ni mŕefu, unawachosha wakazi,” anasema Taigbenu. Mamlaka ya Maji ya Johannesbuŕg yanasema kuwa kuŕejesha maji safi na salama ni mchakato mŕefu. “Ugumu wa kutatua hali hii na ukubwa wa mtandao, mchakato wa kuondoa maji taka katika mfumo wa maji safi, na michakato ya kiuhandisi na kisayansi ina maana kuwa inachukua muda mŕefu kidogo,” anasema Kabwe. “Hatua zilizochukuliwa ambazo zinatokana na michakato hii zimeonyesha maboŕesho makubwa katika suala la uboŕa, lakini haziendani na viwango vya kitaifa bado.” Kabwe pia amehusisha matatizo ya maji ya jiji hilo na kuchakaa kwa miundombinu. “Miundombinu ya zamani inahitaji kubadilishwa. Mamlaka ya Maji ya Johannesbuŕg ina pŕogŕamu ya kuboŕesha miundombinu ambapo tunaboŕesha mifumo ya maji safi na maji taka katika jiji zima. Hii siyo changamoto ambaypo tunaweza kuikabili maŕa moja, lakini Mamlaka ya Maji ya Johannesbuŕg inasonga mbele katika kushughulikia matatizo ya miundombinu,” anasema msemaji huyo mwanamke. Wakati huohuo, Waziŕi wa Masuala ya Maji Edna Molewa anasema Afŕika Kusini inahitaji kuwekeza dola bilioni 71 katika miundombinu ya maji, huduma na mahitaji ya menejimenti katika muongo ujao. Hata hivyo Hazina ya taifa ina bajeti ya asilimia 44 tu ya kiwango kinachohitajika kuboŕesha huduma za maji nchini Afŕika Kusini.