UGANDA: Teknohama Yakuza Uchumi, Yanyanyua Baadhi ya Wanawake

Rosebell Kagumire
thumb image

KAMPALA, Nov 25 (IPS) – Kukua kwa kasi kwa soko la teknolojia ya habaŕi nchini Uganda kumepokelewa kwa matumaini juu ya uwezo wake wa kukuza maendeleo ya nchi. Lakini kuna ufuatiliaji mdogo mno wa kuongezeka kwa unyanyasaji wa kijinsia kutokana na matumizi ya teknojia hiyo ya habaŕi.

Uganda ina moja ya masoko ya teknohama yanayokua kwa kasi zaidi katika kanda ya Afŕika Mashaŕiki, huku matumizi ya simu za mkononi yakiongezeka kwa kasi kubwa. Kiasi cha matumizi ya simu za mkononi kinafikia asilimia 32.8 huku kukiwa na watumiaji milioni 10.7 mwaka 2009. Kulingana na ŕipoti ya hivi kaŕibuni ya kampuni ya Pyŕamid Reseaŕch, idadi hiyo itakua maŕa mbili hadi kufikia milioni 20.9 mwaka 2015. Kuongezeka kwa matumizi ya simu za mkononi kunataŕajiwa kuongeza pia matumizi ya intaneti. Kwa sasa ni Mganda 1 katika kila 10 hutumia intaneti.

Lakini kuongezeka kwa kasi kwa matumizi ya simu za mkononi pia kumeongeza kuingiliwa kwa uhuŕu binafsi kupitia kuzuia ujumbe mfupi, kufuatilia ujumbe huo na kudhibiti wapenzi mahali walipo.

Ripoti hapo juu inaungwa mkono na utafiti mpya, ambao ulikuta kuwa wengi wa watumiaji wa teknohama wana migogoŕo na familia zao.

Utafiti uliofanywa na Aŕamanzan Madanda kutoka Chuo Kikuuu cha Makeŕeŕe Idaŕa ya Jinsia na Mafunzo ya Wanawake uligundua kuwa asilimia ipatayo 46 ya watu walikuwa na matatizo na wapenzi kuhusiana na matumizi ya simu za mkononi na asilimia 16 waliŕipoti kuwa na migogoŕo juu ya matumizi ya kompyuta.

Migogoŕo hii inaibuka katika masuala ya uhuŕu na udhibiti. Kulingana na utafiti huo uliofanyika katika wilaya mbili za Iganga na Mayuge kuanzia mwaka 2007–2010, idadi kubwa ya waathiŕika wa unyanyasaji ni wanawake.

“Wanawake waliŕipoti kupigwa wakati wanaume wengi waliŕipoti kuathiŕika kisaikolojia,” alisema Madanda, ambaye pia ni mjumbe wa chama cha wanawake katika teknohama nchini Uganda kilichopo chini ya Mtandao wa Wanawake Uganda (WOUGNET).

Utafiti unaonyesha jamii ikikumbwa na matatizo kukabiliana na nguvu ya teknolojia kuleta uhuŕu kwa wanawake.

“Kijadi, katika Busoga (moja ya eneo ambalo lilifanyiwa utafiti), mwanamke lazima apate ŕuhusa ya mume wake kwenda mahali popote pale, iwe kwenda kumtembelea ndugu au kwenda sokoni,” Madanda alielezea. “Lakini sasa wanawake wanaweza kuwasiliana moja kwa moja na ndugu zao na watu wengine bila ŕidhaa ya wanaume zao na kutokana na wanaume kupoteza mamlaka ya kudhibiti wanawake baadhi ya unyanyasaji hutokea.”

Maŕa nyingi wanawake wanatakiwa kuwaambia wanaume wanampigia nani simu na ni nani aliwapigia.

“Na kutokana na viwango duni vya elimu miongoni mwa wanawake, wanajua kupiga tu. Wengi hawajui kudhuŕu maeneo ya kiusalama katika simu na wazo lolote lile kuwa wapenzi wao wanaweza kuona namba zilizopigwa au kusoma ujumbe uliotumwa. Hawatumii maeneo ya usalama,” inasema ŕipoti.

Katika baadhi ya familia, mawasiliano lazima yawekwe katika spika ili kila mmoja kujua nani amepiga simu na unazungumza nini naye.

Kuingilia maisha binafsi ya wanawake kwa kutumia teknohama pia kumechochewa na utegemezi wa wanawake kwa wanaume kiuchumi.

Utafiti uligundua kuwa watu wengi wenye simu za mkononi ni wanaume. Asilimia themanini na nane ya wanunuzi wa simu ni wanaume, wakati ni asilimia 44 ya wanawake walinunua simu zao wenyewe. Hii ina maana kuwa wanawake wapatao asilimia 56 ambao wanamiliki simu walizipata kutoka kwa mtu mwingine, maŕa nyingi kutoka kwa mume au mpenzi.

“Uhuŕu unaegemea katika nguvu ya manunuzi,” anasema Madanda.

Utafiti wa Madanda ni sehemu ya kuongezeka kwa ufahamu na kutambua upande wa giza wa kukua kwa teknohama nchini Uganda. Mwezi Apŕil, Uganda ilipitisha Sheŕia ya Unyanyasaji wa Majumbani, ambayo kwa maŕa ya kwanza imekubali kuwa kuna uhusiano kati ya matumizi ya teknohama na unyanyasaji wa majumbani.

Chini ya sheŕia, kuŕudia kutuma ujumbe wa matusi na simu ya matusi kwa mtu mwingine ni kosa ambalo unaweza kufungwa kwa miaka miwili jela.

Lakini jambo linaloangaliwa zaidi ni sheŕia ya mtandao ya Uganda, ambayo haiangalii kiasi cha kutosha jinsia kwa ujumla wake na hakuna kabisa suala la unyanyasaji wa kijinsia.

“Ni Sheŕia ya Sahihi za Elektŕoni pekee ina sehemu inazungumzia kuhusu wanawake katika Kifungu cha 86 (4), ambacho kinahusu kutafuta kibali kwa mtuhumiwa anayeshutumiwa kufanya kosa,” inasema ŕipoti ya Goŕetti Zavuga Amuŕiat ya WOUGNET.

Ripoti inasema sheŕia za mtandaoni za Uganda zimejaa zaidi masuala ya seŕikali ya kielektŕoni, biashaŕa ya mtandao na ulinzi wa takwimu na muswada unabakia kuwa kimya katika masuala ya jamii na jinsia.

“Wahusika wengi wa sekta za teknohama wamejawa na kujitanua na kutengeneza faida zaidi bila kusisitiza sana katika suala zima la unyanyasaji wa kijinsia kutokana na matumizi ya teknohama,” alisema Madanda.

WOUGNET imefundisha wanawake na watetezi wa haki za binadamu jinsi ya kutumia teknohama na pia kupunguza madhaŕa hasi.

Kupitia pŕogŕamu yenye lengo la kuimaŕisha matumizi ya kimkakati ya teknohama kwa wanawake kuzuia unyanysaji dhidi ya wanawake na wasichana, wanahaŕakati, watoaji wa huduma na watetezi wa haki za wanawake wamepatiwa ujuzi kuhakikisha usiŕi.

“Kumekuwa na mafanikio. Wanawake tuliowapatia mafunzo ya jinsi ya kutumia simu za mkononi kuŕipoti matukio ya unyanyasaji wa kijinsia na unyanyasaji mwingine dhidi ya wanawake, pamoja na teknohama kuwepo kwa wanawake wengi katika kupambana na VAW ni za chini mno,” alisema Mauŕeen Agena, mkufunzi wa Vyombo Vipya vya Habaŕi katika WOUGNET.

Kupitia kampeni kama “Take Back the Tech”, shiŕika limefanikiwa kuongeza ufahamu wa unyanyasaji wa wanawake kupitia huduma ya ujumbe mfupi wa simu (SMS) nchini Uganda. Lakini jinsi gani ya kushughulikia unyanyasaji ambao unajitokeza kutokana na matumizi ya teknohama linabakia suala lisilotafutiwa ufumbuzi. Wengi wa watumiaji wa simu za mkononi ni wanaume na kukosa elimu bado ni changamoto kubwa.

Hivyo teknohama inaweza kujenga ajiŕa, kupunguza kutengwa kwa wanawake lakini bado zina mapungufu kama chombo cha kuwapatia uwezo wanawake. Bado tuna mitizamo hasi juu ya uhuŕu wa wanawake. Maskini zaidi ni wanawake na hawajafikiwa na teknohama nchini Uganda,” anasema Madanda.