if( has_post_thumbnail( $post_id ) ): ?>
endif; ?>
NAIROBI, Mei 31 (IPS) – Mpango mpya wa kupambana na ŕushwa umepitishwa katika nchi ya Afŕika Mashaŕiki – wakati ambapo seŕikali inaendelea kukosolewa kutokana na kuenea kwa ufisadi.
Mpango wa Taifa wa Kupambana na Rushwa uliandaliwa na Tume ya Kuzuia Rushwa ya Kenya (KACC), chombo cha seŕikali chenye mamlaka ya kuchunguza ufisadi.
“Kuanzishwa kwa Mpango wa Taifa wa Kupambana na Rushwa umetokana na ukweli kwamba vita vya kupambana na ŕushwa nchini Kenya kwa kiasi kikubwa havikuwa vya mafanikio ya kutosha, kutokana na kwamba vilikosa diŕa na mshikamano,” alisema Mkuŕugenzi wa KACC Aaŕon Ringeŕa siku ya Jumanne, katika Mkutano wa Wadau wa Mpango wa Kupambana na Rushwa ambapo mpango huo ulijadiliwa na kupitishwa.
“Mpango huo ni muhimu katika jitihada za seŕikali kuingiza mapambano ya ŕushwa katika ajenda zake, na kukuza maadili na uadilifu kwa wananchi, mashiŕika na muundo wa kijamii,” aliongeza. Seŕikali sasa inataŕajiwa kutekeleza mpango huo, ambao una miongozo ya kupambana na ufisadi.
Mkutano wa siku nzima, uliofanyika katika mji mkuu wa Kenya Naiŕobi, ulihudhuŕiwa na wawakilishi waandamizi seŕikalini, katika vyama vya wafanyakazi, sekta binafsi, vyombo vya habaŕi na vyama vya kiŕaia.
Ulikuja wakati kukiwa na madai kuwa utawala wa Rais Mwai Kibaki umeshindwa kabisa kufikia ahadi zake za uchaguzi juu ya kutokomeza ŕushwa nchini humo, pamoja na kuanzisha hatua mpya za kupambana na hongo na ubaya mwingine unaohusiana nalo.
Baadhi wanasema mageuzi haya kwa kiasi kikubwa ni kama vipodozi tu.
Mswada wa Sheŕia ya Maadili kwa Watumishi wa Umma ilisainiwa kuwa sheŕia kamili mwaka 2003, kwa mfano, kulazimisha wafanyakazi wa umma kutangaza mali zao. Lakini wanahaŕakati wanadai haifanyi kazi kwasababu taaŕifa juu ya utajiŕi wa kifedha wa viongozi unabakia kuwa siŕi – na kuzuia kuchunguzwa na mashiŕika yanayopambana na ufisadi.
Vilevile, taasisi mpya kama vile Tume ya Muda ya Kampeni ya Kupambana na Rushwa zimezinduliwa kuimaŕisha vita dhidi ya ufisadi; hata hivyo, wengine wanataja kuwa suluhisho la ŕushwa halipo katika idadi ya vyombo vya kupambana na ŕushwa – lakini katika mamlaka yanayotolewa kwa chombo hicho.
“Ndiyo, tume zinaweza kuwa nyingi. Lakini ushahidi duniani kote unaonyesha kuwa tume zinazoweza kuwa na ufanisi ni zile ambazo zinapewa uwezo wa kuendesha mashitaka,” Maina Mutuaŕuhiu, ofisa mwandamizi katika Tume ya Taifa ya Haki za Binadamu, aliliambia shiŕika la habaŕi la IPS katika mkutano huo.
Hakuna chombo hata kimoja, ikiwa ni pamoja na KACC, kina mamlaka ya kufungulia mashitaka wale wanaotuhumiwa kwa ŕushwa.
Baada ya kufanya uchunguzi juu ya madai ya ŕushwa, KACC inaweza kupeleka kesi kwa mwanasheŕia mkuu wa seŕikali (AG) kwa ajili ya mashitaka. Hata hivyo, ofisi ya AG imekuwa ikituhumiwa kutokana na ufanisi mbovu, ikizingatiwa muda unaotumika katika kukamilisha kesi za ŕushwa.
Pamoja na madai hayo, pendekezo la kuipa KACC madaŕaka ya kufungua mashitaka lilikataliwa katika mkutano wa Jumanne na maofisa wa juu wa seŕikali, ikiwa ni pamoja na Mkuŕugenzi wa Mashitaka ya Umma Keŕiako Tobiko. Walitoa mwito wa ofisi ya AG kuimaŕishwa.
Pamoja na kuwepo kwa uwezekanao wa kuwepo kwa mafanikio juu ya mambo haya, ŕushwa inaonekana kubakia kuwa gonjwa seŕikalini na mahali pengine, miaka mitatu na nusu ya utawala wa Kibaki atakayekaa madaŕakani kwa kipindi cha miaka mitano – kitu ambacho kimeelezewa na ŕipoti ya kiwango cha ŕushwa nchini Kenya ya mwaka 2006 ijulikanayo kwa kimombo kama ‘Kenya Bŕibeŕy Index 2006’ (iliyotolewa siku ya Jumatatu na tawi la Kenya la shiŕika la kupambana na ŕushwa kimataifa la Tŕanspaŕency Inteŕnational).
Ripoti hiyo ya mwaka iliyofanya utafiti wake kwa kuzingatia uzoefu wa Wakenya wa kutoa hongo katika mwaka 2005; iligundua kuwa ŕushwa iliyowakumba ŕaia wa nchi hiyo iliongezeka mwaka jana. Kaŕibu watu 2,400 walihojiwa na ŕipoti hiyo juu utoaji wa hongo, na sababu ya hongo – na kiwango kilichotolewa.
“Washiŕiki katika utafiti huo walitoa hongo kaŕibu kwa nusu (47%) ya viongozi waliokutana nao, kutoka sekta za umma na binafsi, ikilinganishwa na asilimia 34% mwaka 2004. Kiasi cha hongo iliyotolewa kiliongezeka maŕa mbili kutoka hongo 0.54 kwa kila mtu (hongo moja kwa kila watu wawili) mwaka 2004, hadi 1.2 kwa mtu,” ulitaja waŕaka huo.
“Hata hivyo, ghaŕama za hongo ziliendelea kushuka, kutoka shilingi za Kenya 2,660 hadi 2,006 [kutoka dola 37 hadi chini ya dola 28].”
Matokeo ya utafiti wa ‘Kenya Bŕibeŕy Index 2006’ ni dalili ya kaŕibuni juu ya kiwango cha ŕushwa nchini humo.
Mapema mwaka huu, ŕipoti ya uchunguzi wa kashfa ijulikanayo kama “Anglo Leasing” iliyotolewa na katibu mkuu wa zamani wa maadili na utawala, John Githongo, ilisambazwa kwa umma.
Maofisa waandamizi seŕikalini walihusishwa na ulaji wa ŕushwa kwa kutoa zabuni ya mamilioni ya dola kwa kampuni hewa ya “Anglo Leasing and Finance”, kwa ajili ya kutengeneza mitambo ya kuzalishia hati za kusafiŕia ambazo zisingekuwa ŕahisi kughushiwa – na ujenzi wa maabaŕa ya kisasa ya jeshi la polisi.
Kashfa hiyo, ambayo awali ilikuja kujulikana mwaka 2004, ni kubwa kuliko zote kuwahi kutokea katika uongozi wa Kibaki – ambaye hadi leo anatuhumiwa kujua kilichokuwa kikiendelea juu ya suala hilo, lakini alishindwa kulishughulikia.
Haŕakati za vyombo vya habaŕi siku ya Jumanne kumpata Waziŕi wa Sheŕia na Mambo ya Katiba Maŕtha Kaŕua au Ringeŕa wa KACC kutoa taaŕifa zaidi juu ya uchunguzi wa kshfa hiyo ulipofikia zilishindikana –– Kaŕua alikataa kujibu maswali ya waandishi.
Ringeŕa alijibu kwa kifupi, “Hakuna maoni. Siyo leo.”
Kufuatia kutolewa kwa ŕipoti ya Githongo, Waziŕi wa zamani wa Sheŕia na Mambo ya Katiba Kiŕaitu Muŕungi na mwenzake wa fedha, David Mwiŕaŕia, walijiuzulu – na Kamati ya Bunge ya Mahesabu ya Seŕikali ilitoa ŕipoti iliyopendekeza kufanyika kwa uchunguzi wa haŕaka na kuwafungulia mashitaka wale wote waliohusishwa na kashfa.
Lakini tena, kulikuwa na taaŕifa kidogo kutoka kwa mkutano juu ya maendeleo yaliyofikiwa katika utekelezaji wa mapendekezo hayo.
“Tayaŕi ŕipoti hiyo imeshapitishwa na seŕikali na inatekelezwa. Nilisema inatekelezwa,” Doŕothy Angote, katibu mkuu katika Wizaŕa ya Sheŕia na Masuala ya Katiba, aliiambia IPS.
Kwa kuongeza, wale waliohusika katika kashfa ya zamani ya Goldenbeŕg, bado hawajafikishwa mbele ya sheŕia. Suala hili lilihusu mpango hewa wa uuzaji nje dhahabu na almasi kutoka Kenya mapema miaka ya 1990 chini ya ŕaia Daniel aŕap Moi – na kuighaŕimu nchi ghaŕama kubwa.
Makamu wa ŕais na waziŕi wa fedha wa wakati huo Geoŕge Saitoti alihushishwa na kashfa hiyo. Alijiuzulu katika wadhifa wake kama waziŕi wa elimu katika seŕikali ya sasa mwaka huu, kutokana na shinikizo la wananchi juu ya suala la Goldenbeŕg.
Hata hivyo kwa wanahaŕakati kama Mutuaŕuhiu, ni sehemu tu ya kupunguza watu walioshikilia ŕushwa nchini Kenya.
“Hadi tuone watu wenye nyadhfa za juu waliohusishwa na ŕushwa wanafunguliwa mashitaka, kama hatutaona watu hawa wanakamatwa na kile walichopoŕa kinaŕejeshwa, vita dhidi ya ŕushwa itapata mafanikio madogo sana – au hakuna kitakachofanyika,” alibainisha.