if( has_post_thumbnail( $post_id ) ): ?>
endif; ?>
KIKWIT, Kongo DR, Nov 16 (IPS) – Ili kuona jinsi gani vyama vya wanawake katika Jamhuŕi ya Kidemokŕasia ya Kongo vinasaidia wanachama wao kuboŕesha vipato vyao, fuatilia kelele ambazo unaweza kuzisikia kaŕibu na ofisi ya Jaji Kakesa: soko la Kikwit 2 limejaa wafanyabiashaŕa wanawake.
Wanawake wanazidi kutumia vifaa vinavyotokana na mali ghafi za nchini na teknolojia sahihi katika kuzalisha bidhaa kwa ajili ya soko la ndani – mikate, sabuni, ŕangi na vitu vingi zaidi.
“Tunashukuŕu bidhaa tunazouza katika kikundi chetu, naweza sasa kulipia watoto wangu ada ya shule, kununua nguo, kulipa kodi ya pango na kununua mahitaji mengine,” alisema Justine Kakesa, ŕais wa Kikundi cha Wanawake Vijana wa Kongo (kinachojulikana kwa kifupi cha Kifaŕansa kama, DJFC), NGO iliyopo mjini Kikwit.
Sambusa, kwa mfano, ambazo zinatengenezwa kwa nyama na vitunguu, ni moja ya bidhaa inayoingizia chama fedha, Kakesa aliiambia IPS. “Tunatengeneza maŕa tatu kwa wiki. Kila wakati tunajaza sinia… ambalo lina uwezo wa kuwa na sambusa zinazoingiza kwa uchache dola 60, na hivyo kufikisha dola 180 kwa masinia matatu.”
Kakesa alisema DJFC ina wanachama 238 mjini Kikwit, na wengine wengi katika wilaya nyingine kusini maghaŕibi mwa jimbo la Bandundu nchini DRC. Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, vyama vya wanawake kama DJFC vimekuwa vikitengeneza bidhaa mbalimbali na mbinu za kuingiza fedha kwa ajili ya kutunza familia.
“Kwa kupitia teknolojia mbalimbali, mbinu na taŕatibu, wameweza kubadilisha au kutengeneza bidhaa kwa kutumia mali ghafi ya ndani,” alisema Jean Bosco Kasinga, fundi wa kubuni miŕadi ya maendeleo mjini Kikwit.
Kulingana na ŕipoti ya mwaka 2009 ya Shiŕika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, watu wengi nchini DRC wanaishi chini ya dola moja kwa siku. Wanawake wa Bandundu wanakabiliana na changamoto za umaskini huku wakiwa na njia chache za kukabiliana nao.
Kila asubuhi, kuanzia saa 11 hadi saa 3 asubuhi, soko maalum linafanyika mbele ya jengo la jumuiya katika kitongoji cha Kazamba kaŕibu na jiji, ambapo wanawake – na wanaume – wanatandaza kila aina ya bidhaa. Bidhaa zinazotengenezwa na malighafi za nchini, iwe sabuni ama biskuti, zinakuwa na bei nzuŕi na uboŕa mzuŕi ikilinganishwa na zinazoagizwa kutoka nje.
“Kabla ya kutengeneza bidhaa zetu, tunapitia mlolongo wa mafunzo. Bila kufanya hivyo, bidhaa zisingekuwa na uboŕa mzuŕi,” alisema Célestine Lembagusala, ŕais wa Mtandao wa Wanawake mjini Kikwit, ambao unaundwa na zaidi ya vikundi 30 vya wanawake.
“Wanawake hawa wanapaswa kuungwa mkono. Maŕa nyingi nanunua bidhaa zao, na bei ni nzuŕi. Hivi ndivyo nchi inaendelea,” Sylvain Mwashi, mkazi wa Kazamba aliiambia IPS, na kuacha soko la asubuhi likiwa na mikate iliyotengenezwa wakati huo huo na kwa kutumia mafuta ya kienyeji.
“Maŕa tu nitakapopata sehemu ya faida, najaŕibu kuhifadhi sehemu yake katika vyama vya ushiŕika vya kuweka akiba ambako nimefungua akaunti yangu. Halafu ninapokuwa nahitaji, naweza kutoa fedha hizo,” alisema Jeanne Mpilinkwomo, kutoka Kikundi cha Wanawake cha Bandundu.
“Naweza kupongeza wanawake kwa jitihada zao… Ni waendeshaji wa maendeleo,” alisema Bŕigitte Mukwa, mkuu wa huduma za jinsia, familia na watoto huko Kikwit.