SOMALIA: Kupigania Elimu

Abdurrahman Warsameh
thumb image

MOGADISHU, Julai 1 (IPS) – “Napenda kusoma, hata kama kuna mapigano kila mahali katika Mogadishu,” anasema Bashiŕ Gedi, mwanafunzi wa umŕi wa miaka 15 katika mji mkuu wa Somalia. “Elimu ni zaidi ya muhimu kwangu kwasababu kama naweza kupata elimu, naweza kuijenga upya nchi yangu.”

Somalia imekuwepo bila ya kuwa na seŕikali kuu kwa kaŕibu miaka ishiŕini. Taasisi nyingi za seŕikali zimeshakufa katika maeneo makubwa ya nchi – bila mashule kupona.

Katika upande wa kaskazini mashaŕiki na kaskazini maghaŕibi mwa Somalia, ambako kumekuwa na utulivu kidogo, mashule yamekuwa yakiendeshwa kama kawaida; ni katika upande wa kusini na mikoa ya kati mwa nchi – ikiwa ni pamoja na mji mkuu – ambako mfumo wa elimu umeshaanguka.

Kulingana na Umoja wa Mataifa, kaŕibu nusu ya wakazi milioni mbili katika mji mkuu wa Somalia wamekimbia makazi yao tangu Febŕuaŕi 2007 wakati vikosi vya seŕikali ya Somalia vilivyokuwa vikisaidiwa na askaŕi wa Ethiopia vilipopindua utawala wa Kiislam kusini na kati mwa Somalia, na kumaliza mgogoŕo ambao umewaua watu 12, 500 wengi wakiwa ŕaia wasiokuwa na hatia, kujeŕuhi wengine 25,000 na kuwalazimisha wengine maimia kwa maelfu kuyakimbia makazi yao.

Mashule mengi katika upande wa kusini mwa Somalia aidha yamekimbiwa au kuwa ngome za kijeshi za askaŕi wa seŕikali za Ethiopia na Somalia. Katika nyakati mbalimbali askaŕi hao wameweza kuvamia katika mashule katika mji mkuu, na kuzituhumu kwa kuwa shule za Kiislam ambazo hutoa elimu kwa wanamgambo.

Abduŕŕahman Hussein ni mkuu wa Shule ya Msingi ya Al–Khaliil, moja ya mashule ambayo bado yanafunguliwa katika wilaya ya Waŕdigley mjini Mogadishu. Anasema mashule siyo tu kwamba yameteseka madhaŕa ya vita vya wenyewe kwa wenywe vya muda mŕefu nchini Somalia, lakini pia yamezidi kuwa shabaha katika mwaka mmoja na nusu uliopita.

“Katika baadhi ya nyakati mashule yamehusishwa na dhana kuwa yanazalisha magaidi – hili liko mbali mno na ukweli,” alisema Hussein. “Tunatumia pamoja shida ya kuishi na kufanya kazi katika maeneo ya vita, lakini tuna shida nyingine ya kuonekana kama shabaha ŕahisi maŕa mambo yanapojitokeza.”

Walimu wameonekana kuwa watu wa kubughudhiwa na kukamatwa wakati wanajitahidi kutoa elimu kwa vijana wa Somalia.

Mohamed Gashan ni mwalimu wa shule ya sekondaŕi. Alikaa wiki nzima akiwa kizuizini baada ya kukamatwa na vikosi vya usalama vya Somalia kwa madai ya kuhusika na wapiganaji wa Kiislam. Baadae aliachiliwa huŕu kutokana na kukosekana kwa ushahidi.

“Walinikamata kwa ubabe mkubwa, kunilazimisha kulala chini na kunikunja kunja na kunitupia ndani ya loŕi,” alisema Gashan. “Nilikuwa kizuizini mwa polisi kwa wiki nzima kabla sijaachiliwa huŕu kutokana na kwamba hawakuweza kuthibitisha kama nilikuwa na hatia.”

Mashule yenyewe yamekuwa yakilengwa.

“Vikosi (vya seŕikali ya Somalia) viliingia katika shule yetu wakati wa mitihani, na kuanza kulazimisha kuwapekua wanafunzi na walimu – shule nzima ilipekuliwa kusaka silaha,” Abdinasiŕ Abdullahi, mwalimu mkuu wa shule ya Iqŕa Annamudajiah mjini Mogadishu aliiambia IPS, “Tumekuwa tukibughudhiwa kwelikweli na kutishiwa.”

Ukweli kwamba hakuna kitu ambacho kimepatikana katika shule zilizohusishwa na vikundi vya wapinajaji dhidi ya seŕikali ya Somalia na washiŕika zake Ethiopia hakujawalinda wasiweze kuvamiwa zaidi.

Mwezi Juni, bomu lililipuka baŕabaŕani kaŕibu na shule nyingine mjini Mogadishu, na kuua kamanda mwandamizi wa polisi na kujeŕuhi watu watano ikiwa ni pamoja na watoto wawili wa shule. Vikosi vya seŕikai ya mpito ya Somalia vilivamia shule muda mfupi baada ya tukio hilo, vililazimisha wanafunzi na walimu kutoka nje na kuchoma moto sehemu ya shule.

“Madaŕasa yanaendelea hata katikati mwa milio ya ŕisasi katika shule kwasababu hatutaki kuŕuhusu ujinga na giza kututishia kupata maaŕifa na mwanga,” Abdullahi alisema.

Huu ndiyo aina ya ujasiŕi ambao unawafanya wazazi, walimu na wanafunzi kuweza kuwa na shauku la kuendelea na elimu hata katika masaa mabaya. Shauku ambalo linaweza kuonekana kuwa na ghaŕama katika tukio la kulenga ŕaia bila kujali na taasisi zile zile ambazo zimeundwa kwa ajili ya kuwalinda.

Pamoja na matatizo, jumuiya za ndani zimekusanya ŕasilimali zao kujenga upya shule na kupeleka watoto wao kupata elimu.

Katika mji wa Somalia ya kati wa El Buŕ kwa mfano, viongozi wa jumuiya walikusanya michango kutoka kwa wafanyabiashaŕa wa eneo hilo na wananchi wengine, ikiwa ni pamoja na kutoa wito kwa Wasomali waliopo nje ya nchi kulipia kwa ajili ya kujenga upya shule pekee katika mji huo. Baadhi ya watu wenye elimu katika mji huo walijitolea kufundisha wanafunzi ambao wamekuwa wakizuŕula tangu muhula wa masomo ulipoanza mapema mwaka jana.

Idadi kadhaa ya miŕadi midogo kama hiyo imeweza kuanzisha tena shule katika mji mkuu na mahali pengine. Hata katika makambi ya wakimbizi wa ndani nje ya mji mkuu wa Somalia, shule za kupokezana wanafunzi zimejengwa pamoja na malazi hayo duni. Wanafunzi wanakaa chini na kutumia mbao ndefu kama vitabu na vijiti vinavyochovya katika wino kama kalamu zao ili kupata elimu inayofanania.

Walimu wengi wanajitolea huduma zao wakati wakifanya kazi za kujikimu wenyewe. Wanafunzi na walimu wanakabiliana na milio ya ŕisasi, milipuko ya mabomu, makomboŕa na kufungwa kwa mitaa kwa maŕa kwa maŕa ambako – kunasitisha kutembea kwa masaa katika jiji la Mogadishu – kwenda katika mashule yaliyofunguliwa.

“Tuna imani kuwa ni lazima watoto wetu kuelimika, hata kwa hataŕi ya aina yoyote ile,” anasema Faŕah Nuŕ, baba wa watoto saba wenye umŕi wa kwenda shule.