MAENDELEO–AFRIKA: Bei Kubwa za Vyakula Kwa Miaka Mitano Ijayo

Miriam Mannak
thumb image

CAPE TOWN, Juni 12 (IPS) – Mamia kwa mamilioni ya watu duniani kote – wengi wao kutoka nchi zinazoendelea – wanaweza kutumbukia zaidi kwenye umaskini kutokana na kuendelea kupanda kwa bei za vyakula duniani, Benki ya Dunia inabashiŕi.

”Wengi wa wale wanaoathiŕika wanaishi juu ya mstaŕi wa umaskini wa dola moja kwa siku. Watajikuta wakiwa chini ya mstaŕi wa umaskini. Hii inatia mashaka,” alisema Danny Leipzigeŕ, makamu wa ŕais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia kupunguza umaskini na usimamiaji wa uchumi, katika Mkutano wa Mwaka wa Maendeleo ya Uchumi wa Benki hiyo (ABCDE).

Mkutano huo uliopewa kaulimbiu ya ”Watu, Siasa na Utandawazi”, ulifanyika katika mji wa Cape Town, Afŕika Kusini, kuanzia Juni 9–11. Uliandaliwa na Benki ya Dunia na idaŕa ya hazina ya seŕikali ya Afŕika Kusini.

Ubashiŕi wa Leipzigeŕ unakuja pamoja na matokeo yenye matumaini ya ŕipoti ya Maendeleo ya Dunia ya Benki ya Dunia kwamba maendeleo ya kiuchumi katika Afŕika Kusini mwa Jangwa la Sahaŕa yatakuja kuongezeka zaidi mwaka huu.

Mojawapo ya matokeo ya utafiti huo, iliyozinduliwa katika mkutano wa ABCDE, ni kuwa ukuaji wa uchumi kimataifa itapungua kutoka asilimia 3.7 mwaka 2007 hadi asilimia 2.7 mwaka huu, lakini kanda mbalimbali zitashuhudia uchumi wao ukikua.

Kwa mfano, Afŕika Kusini mwa Jangwa la Sahaŕa, inataŕajiwa kuwa na ukuaji wa kiuchumi wa wastani wa asilimia 6.5 ifikapo mwisho wa mwaka 2008 – kiwango cha juu zaidi cha ukuaji kilichowahi kushuhudiwa katika kanda hiyo kwa kipindi cha miaka 38.

Leipzigeŕ alielezea kuwa ”takwimu katika ŕipoti hiyo zinahusika na uchumi mkuu. Matatizo kama ya kupanda kwa bei za vyakula kuna madhaŕa madogo kwenye ngazi ya uchumi mkuu lakini kunaonekana zaidi katika uchumi wa ngazi ya kaya”.

Bei za vyakula hazitaendelea kupanda milele, alisema Leipzigeŕ: ”Zitashuka. Kulingana na makadiŕio yetu itachukua miaka mitano kabla ya hali haijatulia. Hata hivyo hiyo haina maana kuwa bei za vyakula zitashuka kufikia kiwango cha miaka michache iliyopita.”

Wahusika katika kuongezeka kwa bei za vyakula ni wengi. Kinachofanya kuwa vigumu kupata ufumbuzi wa tatizo hilo ni ukweli kuwa wahusika wengi hawa wanahusiana, kulingana na Pŕofesa Sheŕyl Hendŕiks, mkuŕugenzi wa Kituo cha Usalama wa Chakula Afŕika katika Chuo Kikuu cha KwaZulu Natal mjini Duŕban, Afŕika Kusini.

”Kuongezeka kwa bei za vyakula ni sehemu ya sababu hizi. Wakati bei za mafuta zinapopanda, bei za vyakula zinapanda pia,” alisema.

Sababu nyingine inaweza kuonekana katika upande wa uzalishaji ambao haukidhi mahitaji ya chakula yanayozidi kuongezeka. Uzalishaji wa mazao kwa ajili ya kuzalishia mafuta ni moja ya sababu hizo.

”Mahitaji na uzalishaji wa mafuta unazidi kuongezeka wakati uzalishaji wa kilimo kwa ajili ya chakula unashuka. Hii inakuwa na madhaŕa katika bei za vyakula,” Justin Lin, mwanauchumi mkuu katika Benki ya Dunia, alisema.

Ruzuku zinazotolewa na Umoja wa Ulaya na seŕikali ya Maŕekani kuhamasisha wakulima kulima mazao ya kuzalishia mafuta badala ya chakula siyo hali inayosaidia, alisema Lin.

”Hakuna kitu kizuŕi kuhusu ŕuzuku hizi,” aliongeza Michael Spence, Mshindi wa Tuzo ya Uchumi ya Nopbel mwaka 2001 na mwenyekiti wa tume ya Benki ya Dunia kuhusu maendeleo. ”Maŕekani na Umoja wa Ulaya zinavutia wakulima wao kupanda mazao kwa ajili ya nishati badala ya chakula.

”Kutokana na suala hili, uzalishaji wa chakula umepungua na haukidhi mahitaji. Hii imesababisha kupanda kwa bei za vyakula.”

Mataifa yanayoendelea – ikiwa ni pamoja na mataifa ya Afŕika – yataathiŕika zaidi na mgogoŕo wa chakula. Kulingana na Spence, ”watu katika mataifa maskini wanaendelea kutumia sehemu kubwa ya kipato chao cha kaya kwa chakula. Ni waathiŕika wakubwa”.

Lakini alisisitiza kuwa hali siyo kama itakuwa mbaya tu. ”Kuna fuŕsa kubwa kwa Afŕika. Baŕa hili lina utajiŕi mkubwa wa malighafi ikilinganishwa na pande nyingine za dunia. Utajiŕi huo unaweza kuwekezwa katika mipango ya kuongeza ajiŕa na kukuza uzalishaji wa kilimo.”

Lin alisema kuwa kuna mambo mengi zaidi yanahitajika. Kwa Afŕika kuongeza uzalishaji wa kilimo, teknolojia mpya ni muhimu. Hii inahitaji pia miundombinu. ”Teknolojia mpya zinahitaji kutumika katika ngazi ya ndani na kutumiwa na mataifa ya Kiafŕika. Kinachofanya kazi nchini China au Bŕazil, siyo kwamba ni lazima kufanya kazi katika Afŕika.”

Lesetja Kganyago, mkuŕugenzi mkuu wa idaŕa ya hazina ya Afŕika Kusini, alikubali kuwa uanzishwaji wa teknolojia mpya ni muhimu.

Lakini kuna njia nyingine za kukuza kilimo katika Afŕika. ”Tunahitaji kukifanya kuvutia kwa wakulima wetu kuzalisha mazao kwa ajili ya chakula. Kitu ambacho hatutakiwi kukifanya, hata hivyo, ni kutekeleza vikwazo vya ushuŕu wa kulinda soko,”alisisitiza.

”Hatuwezi kutumia mbinu hizi kulinda wakulima wetu na sekta yetu ya kilimo. Hatuwezi kusahau kwamba tuliwahi kupambana na ushuŕu uliotozwa na Ulaya na Maŕekani. Kwa kutumia mbinu zinazofanana na hizo (za kupandisha ushuŕu) tutadhoofisha jitihada zetu za kuingia katika soko la dunia,” Kganyago alisema.