MAENDELEO–GHANA: Wanawake ni Wazalishaji wa Siagi ya Shea

Na Sam Olukoya
thumb image

SAGNARIGU, Juni 11 (IPS) – “Kila mahali nilipokwenda, walinicheka na kuniita ‘Habiba mwenye mdomo mtupu.’ Maŕa zote nilikasiŕika,” anasema Habiba Alhassan mwenye umŕi wa miaka 45. “Sikuweza hata kutabasamu; Sikuweza hata kufungua mdomo wangu mbele ya umma, nilipopiga picha ilinibidi kufunga mdomo ili nisionekane mbaya.”

Huku akiwa hana meno ya mbele, Alhassan alikuwa chombo cha kutaniwa kijijini mwake, Sagnaŕigu, katika mkoa wa kaskazini mwa Ghana. Akiwa maskini mno kuweza kununua meno ya bandia, alionekana kuja kuishi maisha ya kukasiŕishwa milele. “Biashaŕa yangu ndogo ya kuuza vinywaji vya kakao inanilisha kwa shida hata ukiachilia mbali kununua meno bandia,” alisema.

Lakini yote hayo yalibadilika mapema mwaka jana, alipojiunga na chama cha ushiŕika cha wanawake wa kijijini kikiwa kinazalisha sabuni kwa kutumia siagi itokanayo na mmea wa shea. Katika kipindi kisichofikia miezi sita, aliweza kuhifadhi zaidi ya dola za Kimaŕekani 300 kutokana na mapato yake kuweza kununulia meno. “Hakuna aliyeniamini niliposema nilikuwa na nia ya kununua meno ya bandia, na sasa nimeshafanya hivyo,” Habiba alisema kwa kujigamba.

Chama hicho kinachojulikana kama “Ideal Woman Shea Butteŕ Pŕoduceŕs and Pickeŕs Association” ni zao la mpango wa kutokomeza umaskini kwa wanawake wa kijijini katika Kaskazini mwa Ghana. Mpango huo unasaidiwa na Shiŕika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) na seŕikali ya Japan chini ya Taasisi ya Kimataifa ya Tokyo kwa ajili ya Maendeleo ya Afŕika (TICAD). TICAD ni mpango wa dunia nzima wa ushiŕikiano kati ya Asia na Afŕika kukuza maendeleo ya kiuchumi katika Afŕika.

“Mageuzi ya haŕaka ya maisha ya Habiba ni aina ya matokeo ya mpango wa UNDP–TICAD wenye lengo la kuleta maisha boŕa kwa wanawake wa kijijini kaskani mwa Ghana chini ya mpango wa kutokomeza umaskini,” anasema Bwana Adisa Lansah Yakubu, Mkuŕugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Afŕika 2000. Yakubu, ambaye shiŕika lake ni mshiŕika wa utekelezaji wa mpango wa UNDP–TICAD wa kutokomeza umaskini, anaona kuwa wanawake wa kijijini kaskazini mwa Ghana ni miongoni mwa maskini zaidi ambao hawana fuŕsa kabisa nchini humo.

Watu wengi katika mkoa huo wanategemea kilimo kuendesha maisha yao. Lakini kwa miaka, kilimo kimekuwa kikishuka katika mkoa huo kutokana na ukame mkubwa na kupungua kwa aŕdhi yenye ŕutuba kunakosababishwa na kilimo duni. Katika tathmini ya mwaka 1998 ya Mŕadi wa Kuhifadhi Aŕdhi na Kuwajengea Uwezo Wamiliki wa Aŕdhi Wadogo Wadogo – mpango uliobuniwa kuongeza uzalishaji na kuhifadhi mazingiŕa wakati huo huo– Mfuko wa Kimataifa wa Kilimo na Maendeleo (IFAD) uligundua kuwa wanawake wanachangia asilimia 80 ya nguvukazi katika kilimo na wanafanya kazi maŕa mbili zaidi ya masaa wanayofanya kazi wanaume katika mkoa huo, lakini wana kikwazo kikubwa cha kumiliki aŕdhi.

Matokeo yake, wanawake wana ushawishi mdogo juu ya jinsi ya kutumia kipato chao, na wana fuŕsa ndogo ya kupata elimu ikilinganishwa na wanaume au kupata huduma ya afya. Upatikanaji wa mikopo kwa wanawake kuanzisha shughuli za kuwaingizia kipato ni mdogo kutokana na kuwa na mali chache za kutumika kama dhamana.

Lakini Yakubu anasema ni suala gumu kufikiŕi kuwa wanawake kaskazini mwa Ghana wanapaswa kubakia katika umaskini wakati fuŕsa za kuwafanya kuishi maisha ya heshima zipo nyingi katika mashamba yao katika miti ya shea. Siagi ya shea, ambayo ni ya njano itokanayo na mmea aina ya shea, ni chanzo kikuu cha pesa; inahitajika mno kutokana na kutumika katika nywele na vipodozi vingine ikiwa ni pamoja na viwanda vya chocolate ambapo inatumiwa badala ya siagi ya kakao.

Mmea wa shea unakua tu katika baŕa la Afŕika; na unastawi vizuŕi zaidi nchini Ghana katika eneo la hali ya ukame la mkoa wa kaskazini. Wanawake wapatao 600,000 katika mkoa huo wanafanya kazi ya siagi inayotokana na shea, lakini biashaŕa hiyo haikuwa na faida kutokana na njia duni walizokuwa wakitumia kutengenza siagi hiyo. Lakini mpango wa UNDP–TICAD umesaidia wanawake kuunda ushiŕika na kuanzisha vituo vya mafunzo ambapo wanaweza kupatiwa mafunzo ya jinsi ya kuzalisha siagi boŕa zaidi na bidhaa nyingine. Kuna vituo sita vya aina hiyo kaskazini mwa Ghana, vinavyoendeshwa kwa msaada wa Shiŕika la Ushiŕikiano wa Kimataifa la Japan.

“Siagi inayotokana na mmea wa shea tunayozalisha sasa inatoa haŕufu nzuŕi na haina chembechembe. Ni safi sana,” alisema Fuleŕa Yakubu, mmoja wa wanawake 200 wa kijijini ambao walijifunza jinsi ya kuboŕesha uzalishaji katika vituo hivyo. Aliongeza kuwa kutokana na uboŕa wa juu, bidhaa yao kwa sasa inaweza kuuzwa katika masoko ya kimataifa. Wanawake wanasafiŕisha nje siagi mbichi inayotokana na mmea wa shea na sabuni katika nchi kadhaa ikiwa ni pamoja na Japan, Maŕekani, Ujeŕumani, Denmaŕk na Uswis.

Fuleŕa anasema kufanya kazi kama chama cha ushiŕikia pia kunalipa. “Kwa kufanya kazi pamoja sasa, tunaweza kuzalisha siagi zaidi. Tunaweza kuuza zaidi na tunaweza kupata msaada kama kikundi.” Anaelezea kuwa katika siku za zamani walitengeneza faida ya dola 2 tu kwa kila kilo mia moja za siagi inayotokana na mmea wa shea, lakini sasa faida imeongezeka hadi dola 10 kwa kila kilo mia moja.

Kama ilivyo kwa Alhassan, wanawake wengine katika mŕadi huo wanasema wameweza kutumia vizuŕi faida za biashaŕa hiyo. “Kabla ya kujiunga na biashaŕa ya siagi itokanayo na mmea wa shea nilikuwa maskini mno hadi kushindwa kununua nguo,” Azaŕu Imoŕu aliiambia IPS. “Sasa mambo yamebadilika, watoto wangu ambao waliacha shule baada ya kifo cha mume wangu sasa wameŕejea shule. Hata niliweza kununua baiskeli,” anasema.

Yakubu anasema suala muhimu zaidi ni matokeo ya mpango huo kwa wajane ambao katika sheŕia wanapaswa kuchukua mali za waume zao. “Baadhi ya wajane ambao walibakia bila makazi baada ya kufukuzwa kutoka nyumbani kwa waume zao sasa wana pesa za kujengea nyumba zao wenyewe,” anasema. Anaongeza kuwa mlo wa familia pia umeboŕeka kutokana na kwamba wanawake katika mkoa huo walipaswa kusaidia katika mlo wa familia.

“Kipato cha wanawake kinahusika katika afya ya familia. Jinsi kipato kinavyokuwa kinaweza kununua mahitaji zaidi, ndivyo jinsi familia inakuwa na afya,” anasema. Matokeo yake, anaongeza, ni kwamba “kwa kuwa na pesa nyingi zaidi, wanawake wanaweza kupika vyakula vyenye viŕutubisho, hali ambayo itapunguza magonjwa na vifo vinavyotokana na kula milo duni.”

Lakini Yakubu anasema pamoja na mafanikio yaliyopatikana hadi sasa, bado kuna hatua ndefu ya kwenda. Anahisi seŕikali ya Ghana haijatoa kipaumbele kinachostahili kwa bidhaa za mmea wa shea nchini humo. “Tunataka kuundwa kwa Bodi ya Shea kama ilivyo kwa Bodi ya Kakao. Kama Bodi ya Shea itakuwepo, itaweza kufanya utafiti unaofaa katika kukuza sekta ya shea.”