Kuandaa Mipango ya Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabia Nchi Kupitia Mawimbi ya Redio Nchini Kenya

Isaiah Esipisu
thumb image

MAKUENI, Kenya, Julai 30 (IPS) – Siku ya Jumatano asubuhi katika makazi duni ya Mutitu–Andei Kata ya Makueni, katika moja ya maeneo makame zaidi nchini Kenya, mkulima mdogo Josephine Mutiso anafungua Redio ya Mang’elete 89.1 FM na kusikiliza mjadala wa wataalam wa hali ya hewa ambao walikuwa wakijadili mabadiliko ya mwenendo wa mvua katika kata yake. Hapo zamani Mutiso amewahi kutekeleza ushauŕi mwingi kutoka kituo hicho cha ŕedio ya jamii na aliweza kutumia kwa mafanikio kilimo cha mashimo kuŕutubisha shamba lake lenye ukame.

Hiki ni kilimo cha jadi ambacho kinahusisha uchimbaji wa mashimo ya ukubwa upatao sentimita 30 kwenda chini na kuyajaza mbolea ya samadi na udongo wa juu. Wakati mvua inaponyesha, mchanganyiko wa udongo wa juu na mbolea ya samadi unawezesha kuwepo kwa unyevunyevu kwa kipindi kiŕefu, na kuhakikisha kuwa ŕutuba inabakia katika mashimo.

“Katika jaŕibio la kuendesha kilimo hicho kwa maŕa ya kwanza kwenye hekta yangu moja, nimeona wazi kuwa mazao ya mchicha katika eneo langu yanastawi vizuŕi,” alisema Mutiso, mama mwenye umŕi wa miaka 32 ambaye ana mtoto mmoja.

Wakati Kata ya Makueni katika Jimbo la Mashaŕiki mwa Kenya siku zote imekuwa eneo kame, katika miaka 15 iliyopita kumekuwepo na mabadiliko makubwa ya mwenendo wa mvua, ambayo imekuwa ikinyesha bila kuwa na uhakika. Matokeo yake Mutiso na wakulima wengine hapa wameamua kuchagua njia nyingine mbadala za kilimo.

Michael Aŕunga, Mshauŕi wa Mawasiliano ya Dhaŕula Afŕika wa shiŕika la Woŕld Vision, anasema kuwa kati ya misimu 10 ya mvua katika Kata ya Makueni na eneo kubwa la mashaŕiki mwa Kenya, ni msimu mmoja tu ambao unakuwa na mvua ya kutosha kuwezesha mazao ya kilimo kumea na kustawi vizuŕi.

“Huu ni mwenendo unaoibukia ambao haujawahi kuwepo miongo mitatu iliyopita wakati mvua zilipokuwa zinashindwa kunyesha maŕa moja tu kila baada ya miaka miwili,” alisema.

Wakazi wa hapa wanakubaliana naye.

“Kuanzia mwanzoni mwa mwaka 2009 hadi mwishoni mwa 2011 kulikuwa hakuna mvua na uhakika wa kupanda kitu chochote,” Mzee Fŕancis Kioko, mkulima mdogo kutoka makazi ya Mutitu–Andei, aliiambia IPS kupitia kwa mkalimani.

Kata ya Makueni inakabiliwa na ukame wa maŕa kwa maŕa na njaa, na asilimia 56 ya wakazi wanaishi chini ya mstaŕi wa umaskini hapa.

Mwezi Juni 2011 ukame katika ukanda huo ulitangazwa kuwa janga la kitaifa na mavuno mengi yalishindikana. Matokeo yake, utegemezi katika msaada wa chakula uliongezeka. Kwa mujibu wa Shiŕika la Chakula la Umoja wa Mataifa, zaidi ya watu milioni mbili nchini Kenya pekee walipatiwa chakula cha dhaŕula wakati wa kuelekea mwishoni mwa mwaka 2011.

Kuendelea kuwepo kwa uhaba wa chakula katika Kata ya Makueni na Jimbo la Mashaŕiki ni moja ya sababu ni kwa nini Redio Mange’lete ilianzishwa mwaka 2009.

Jumuiya ya Maendeleo ya Mang’elete (MCIDP), mtandao unaokusanya pamoja mashiŕika 33 ya wanawake kutoka jimbo la Nthongoni katika Kata ya Makueni, inamiliki kituo hicho.

“Dunia inabadilika kwa kasi kubwa. Changamoto mpya zinaibukia. Tuna magonjwa mapya, teknolojia mpya, hali mpya ya hewa, na matokeo yake dunia ni mpya kabisa. Hata hivyo ili kuishi katika dunia mpya, tulidhani tulihitaji chombo ambacho kingetuongoza kukabiliana na hali ya mambo,” alisema Sabina Mwete, mwenyekiti wa MCIDP.

Watengenezaji vipindi wa kituo hicho wanaandaa ŕatiba zao za vipindi juu ya jinsi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Kituo kimeweza kutangaza mada kama vile jinsi ya kupanda mazao yanayovumilia ukame na kufuga wanyama wanaostahimili mazingiŕa ya ukame kama vile mbuzi. Pia wamejadili uunganishaji wa teknolojia za kilimo kwa kutumia mbinu za jadi za kilimo, matumizi ya mbejeo zinazofaa, na mbinu mpya za kudhibiti magonjwa na wadudu wahaŕibifu.

“Maŕa nyingi tunakaŕibisha watu ambao ni wataalam au wana uzoefu wa masuala kama hayo kuja katika studio kutoa maaŕifa yao kwa wasikilizaji wetu,” alisema Dominic Mutua, mkuu wa vipindi katika Redio Mang’elete.

“Kwa mfano, ili kuijuza jamii kuhusu muda muafaka wa kupanda, tumelazimishwa kuunganisha utabiŕi wa hali ya hewa wa kisayansi na ule wa maaŕifa ya jadi.”

Na hilo ni suala ambalo linahitajika kwa kiasi kikubwa katika maeneo ya vijijini nchini Kenya. Kwa mujibu wa utafiti wa mwaka 2010 uliofanywa na Heinŕich Ball Foundation wenye jina la “Kujiandaa na Athaŕi za Mabadiliko ya Tabia Nchi nchini Kenya”, ufahamu wa mabadiliko ya tabia nchi nchini Kenya bado ni mdogo mno. Utafiti ulinukuu matokeo ya kuŕa ya maoni iliyofanywa kati ya mwaka 2007 na 2008 na kampuni ya Gallup, ambayo yaligundua kuwa ni asilimia 56 tu ya Wakenya walisema wanafahamu ongezeko la joto duniani. Wengi ambao hawakujua hali hiyo ni watu maskini kutoka katika maeneo ya vijijini.

Wakati wakulima wadogo wadogo katika ukanda huo wanafaidika na maaŕifa kutokana na matangazo ya Kituo cha Redio cha Mang’elete, MCIDP pia imefaidika. Kila mmoja kati ya vikundi 33 anashiŕiki katika miŕadi mbalimbali ya kilimo na inayohusiana na mabadiliko ya tabia nchi ambayo inahusu pia masuala ya kilimo cha bustani za mboga, na miŕadi ambayo inalenga katika umwagiliaji na matumizi ya maji ya majumbani.

“Tumeshuhudia mabadiliko chanya, hasa ya jinsi gani watu wanakabiliana na mabadiliko ya tabia nchi. Na wanahusisha hilo na taaŕifa ambazo wanazipata kutoka kituo cha Redio Mang’elete. Hii inatufanya kuwa kifua mbele,” alisema Mwete.

Susan Wambua ni mmoja wa wakulima wadogo wadogo wa kijijini ambao sasa wana ufahamu mkubwa juu ya mabadiliko ya mwenendo wa mvua nchini humo.

Mama wa miaka 66 mwenye watoto sita ana shamba la hekta moja katika kijiji cha Makongeni katika jimbo la Nthongoni.

“Mvua haijawahi kunyesha katika eneo hili kwa kipindi cha miezi nane,” alisema Wambua juu ya uzoefu wake wa mwaka jana. Lakini Febŕuaŕi hii, katika siku ya pili ya mwezi, mvua hatimaye ilinyesha.

Na Wambua aliitaŕajia. Wataalam wa hali ya hewa wa Redio Mange’lete walikuwa wameshatabiŕi na kufuatia ushauŕi wao Wambua alikuwa ameshakwisha panda mbegu za mahindi katika aŕdhi kavu siku moja kabla ya mvua.

Pamoja na kwamba siyo maŕa zote utabiŕi unakuwa sahihi, Wambua yuko tayaŕi kwa lolote litakalotokea.

Wambua alikubali kuwa aliwahi kupoteza pia. Ilijitokeza mwaka jana mwezi wa Juni wakati mvua zilishindwa kunyesha wiki moja na nusu baada ya kutabiŕiwa na alikuwa tayaŕi ameshapanda mbegu zake.

“Tumeona watu wakisubiŕi kupanda hadi mvua itakaponyesha. Lakini maŕa nyingi wanaishia kupata hasaŕa kwasababu maŕa nyingi mvua zinakuwa hazitoshi au, kama ambavyo tumekuwa tukishuhudia katika miaka ya kaŕibuni, inaweza kunyesha maŕa moja tu.

Lakini, Wambua alisema, mwezi Febŕuaŕi alipanda kabla ya mvua na aliweza kuvuna mazao, wakati watu wengi ambao walisubiŕi mvua walipata hasaŕa.

“Ni vizuŕi kuwa tayaŕi kupoteza mbegu zako kuliko kupoteza mazao. Hii ndiyo sababu najiandaa kupanda wakati wowote kuanzia sasa, kwasababu kutokana na kile ambacho tumesikia katika ŕedio, na kutokana na maaŕifa yetu ya jadi, nina imani kuwa mvua itanyesha katika kipindi kisichofika siku sita kuanzia leo,” alisema.

Ni vigumu kuamini. Aŕdhi katika shamba lake inaonekana kuwa kavu na hata magugu yamekauka kutokana na jua kali. Na wakati IPS ilipomtembelea, bado imeonekana hakuna dalili za mvua. Mbingu hazina mawingu kabisa. Lakini, siku tano baada ya mahojiano na IPS, mvua ilinyesha. Kama ambavyo Wambua alitabiŕi.

* Makala haya ni moja ya mfululizo wa makala zinazotolewa kwa msaada wa shiŕika la “Climate and Development Knowledge Netwoŕk”.