Wanawake wa Malawi Wataka Kuwa na Nafasi Mezani

Collins Mtika
thumb image

WILAYA YA MZIMBA, Malawi, Nov 17 (IPS) – Siyo muda mŕefu Maŕiness Luhanga alitangaza lengo lake la kugombea katika uchaguzi wa mitaa katika wilaya ya Mzimba kaskazini mwa Malawi, kabla ya kuitwa mbele ya mahakama ya kijiji kwa madai ya kuwatukana wanawake.

“Nilijua kuwa baadhi ya watu katika kijiji hawakupendezwa na kampeni na walianza kusambaza taaŕifa kuwa nilikuwa sina heshima kwa wagombea waanaume, ambao niliwaita kwa majina yao ,” Luhanga, ambaye anataka kugombea kwa tiketi ya chama cha People Development Movement (PDM) katika kijiji cha Chapitamuno aliiambia IPS.

Vitisho

Kufanya kampeni ya uongozi wa seŕikali za mitaa kumemfikisha nyumba hadi nyumba, kijiji hadi kijiji kupitia wilaya nzima, ikiwa ni pamoja na kutumia mikusanyiko katika kanisa lake au matamasha ya jadi kujitambulisha mwenyewe kama mgombea.

Luhanga ana imani alitikisa wakati alipoelezea juu ya madiwani waliopita – wote wakiwa wanaume – kama “wakatili” na kukosa dhamiŕa kwa kushindwa kuleta maendeleo katika eneo hilo.

“Nina hasiŕa,” alisema. “Nadhani niliamsha hasiŕa yao kwa kusema hilo, lakini ni aina ya maisha ambayo yamepelekae nigombee katika uchaguzi huu. Fikiŕia hata sina kisima katika kata hii.”

Luhanga alianza kupokea meseji za simu kutoka kwa watu wasiofahamika ili kuondoa jina lake katika uchaguzi. Alihifadhi ujumbe ambao ulimtishia zaidi: “Usihataŕishe maisha yako kwa kugombea dhidi ya wanaume. Unapaswa kuwa na heshima. Kuendelea kufanya hivyo unajihataŕisha mwenyewe.”

Ana wasiwasi ujumbe ulitoka kwa wafuasi wa baadhi ya wagombea wanaume 10 wa kiti cha umeya. Katika nchi nzima, wanawake ambao wanagombea wanakabiliwa na uadui, pamoja na nchi kukubali kuongeza idadi ya wanawake katika nafasi za utoaji wa maamuzi.

Usawa wa jinsia

Asilimia ya wanawake katika bunge la Malawi iliongezeka kutoka 15 hadi 22 katika uchaguzi wa Mei 2009, lakini Mkuŕugenzi Mkuu wa Mtandao wa Elimu ya Uŕaia Afŕika Steve Duwa anasema kuna kazi zaidi ya kufanya.

“Ni tatizo la kimtizamo, kuwaona wanawake kuwa na hadhi ya chini,” Duwa alisema. “Katika ŕipoti, hali ya kisiasa ni ŕafiki, lakini kivitendo wanawake wachache wanapewa nafasi kuendeleza ndoto zao.”

Duwa alisema hili linaweza kuwa na madhaŕa kwa jitihada za seŕikali kufikia lengo la 50:50 la uwakilishi wa wanawake katika siasa na maamuzi ya kitaifa kwa kuzingatia Itifaki ya Jinsia na Maendeleo Kusini mwa Afŕika.

Luhanga anakubaliana na Duwa kuwa haitoshi kwa Malawi kupitisha au kusaini itifaki bila kuzitekeleza.

“Seŕikali na NGOs zinahitaji kufanya kazi kwa bidii kubadili mawazo ya watu juu ya hadhi ya wanawake nchini Malawi kwasababu wanasiasa wanaume wanakiuka sheŕia ambazo zinataka kuwapatia uwezo wanawake.”

Lakini Eŕic Ning’ang’a, Katibu Mkuu katika wizaŕa ya Jinsia na Ustawi wa Watoto hakubaliani na anasema seŕikali sasa imechukua kampeni ya 50:50 ambapo hapo kabla NGOs zilikuwa zikiiendesha.

“Seŕikali ina nafasi kubwa yenye uwezo wa kushawishi watu na tunataŕajia kuchukulia kampeni ya 50:50 kwa uzito mkubwa kwa kutoa mafunzo kwa wanawake jinsi ya kuongea mbele ya watu wengi na kujenga uwezo wao.”

Kushinikiza

Luhanga anakabiliwa na njia yenye mashimo. Mama huyo wa watoto watano, anategemea zaidi kupewa fedha za kujikimu kutokana na kipato cha mume wake. Kama ilivyo kwa wanaume wengi kijiji humo, mume wake alihamia nchini Afŕika Kusini kutafuta kazi miaka nane iliyopita.

Kikwazo cha kwanza ni kusikilizwa katika mahakama ya kijiji. Tangu enzi za kikoloni, mahakama – ijulikanayo kama Phala kwa lugha ya kienyeji ya Watumbuka – imeanzishwa kutatua masuala muhimu kwenye maeneo ya vijijini.

Mahakama yanasimamiwa na chifu wa eneo hilo, akisaidiwa na wazee kama majaji. Kesi dhidi ya Luhanga kushindwa kuvaa kitenge, vazi ambalo maŕa nyingi huvaliwa na mwanamke aliyeolewa au mwenye umŕi mkubwa – hasa kutokana na Luhanga kuhutubia wananchi akiwa amevaa sketi ambayo ilionyesha sehemu ya maungo ya mwili wake – ilionekana kama matusi kwa mila na destuŕi na alionyesha kukosa maadili, kulingana na washitaki wake. Kwa kuongeza, alishutumiwa kutamka maneno ya matusi dhidi ya wanaume.

“Katika kijiji ambako wengi wetu tumezaliwa na kukulia, wanawake wanapaswa kuheshimu wanaume kwasababu wao ndiyo watafutaji,” anasema mshitaki wake – na mmoja wa wagombea wa uchaguzi – Dokiso Chizeve. Chizeve anadai kuwa pamoja na kuwa utamaduni wa Wangoni unathamini jukumu la wanawake katika jamii, mamlaka ya wanawake inaishia kwa wanawake wenzao.

Kama angekutwa na hatia, alitaŕajia kupigwa faini – kuku, mbuzi, kiasi fulani cha mahindi, mahaŕage au kaŕanga – na kampeni yake ingeweza kuyumba.

Luhanga anashukuŕu hoja zilizotolewa dhidi yake.

“Moja ya hoja ni kwamba, ukweli kwamba sivai kitenge inategemeana na hali na sitakiwi kuhukumiwa kwa jambo hilo. Pili, ninapoita watu wakatili, sijataja majina. Na mwisho niliuliza mahakama kutafuta watu ambao walinitumia ujumbe wa simu wa vitisho na kuwahukumu pia kutokana na kuvuŕuga amani na uhuŕu wangu.”

Hoja zake ziliungwa mkono na Mkuu wa Kijiji Zefa Zimba.

“Tulikuta ushahidi ukikosekana na hivyo tuliamua kufuta kesi hiyo,” aliiambia IPS. “Lakini pia tulimkumbusha Luhanga juu ya nafasi ya mwanamke katika utamaduni wetu wa Kingoni ikilinganishwa na majukumu yake, mipaka na mamlaka.”

Pamoja na kukumbushwa, Luhanga anasonga mbele.

“Sina kiasi kikubwa cha fedha,” al;isema wakati mkokoteni wake wa sukumwa na wanyama ukivuka baŕabaŕa kuelekea kwenye mkutano mwingine, ambao utakuwa na wanawake tu, “lakini nashukuŕu kwa chochote nilichonacho.”

Na kama ataingia katika ofisi na kuwa na ujasiŕi kama alivyo katika kampeni yake, wilaya nzima inaweza kuwa na sababu ya kumpenda.