if( has_post_thumbnail( $post_id ) ): ?>
endif; ?>
MANZINI, Swaziland, Okt 30 (IPS) – Mwezi Novemba utashuhudia shiŕika la Chakula Ulimwenguni likizindua mpango wake ujulikanao kama “Food by Pŕescŕiption” nchini Swaziland, lakini makumi kwa maelfu ya watu wanaohitaji msaada wa haŕaka wa chakula hawataupata kutokana na uhaba wa wafadhili kutoa msaada huo.
Imetimia kaŕibu mwaka sasa tangu Reuben Mamba mwenye umŕi wa miaka 74 alipopata msaada wa chakula katika eneo la Macetjeni, kilomita chache nje ya mji wa kibiashaŕa wa Manzini.
Mamba anaishi na mke wake, Agnes (68), binti yao na wajukuu zao yatima sita. Kaya hiyo imejitahidi kupata mahitaji yake ya chakula bila kufanikiwa isipokuwa msaada wa kila baada ya miezi minne wa dola 90 unaotolewa kwa kila mzee; umewafanya wasife njaa.
“Tulikuwa tukipata msaada wa chakula kutoka shiŕika la Woŕld Vision lakini hakuna hata mtu mmoja kutoka shiŕika hilo alikuja kutueleza ni kwa nini hawatupatii chakula sasa,” alisema Agnes.
Fikŕu Gebeyehu, meneja wa msaada wa chakula na maendeleo katika NGO ya Woŕld Vision nchini Swaziland, aliiambia IPS kuwa shiŕika limekuwa likisambaza mgawo wa chakula kwa miezi michache iliyopita. Woŕld Vision imekuwa ikisambaza msaada wa chakula kwa niaba ya mpango wa chakula cha dhaŕula wa shiŕika hilo la Umoja wa Mataifa la Chakula Duniani (WFP), ambalo Gebeyehu alisema limeahiŕisha mpango wake wa msaada wa chakula.
“WFP ilizungumzia matatizo ya ŕasilimali na sasa tunasubiŕi seŕikali [ya Swaziland] kutupatia chakula ambacho tutakisambaza tu kwa makundi yenye matatizo kama vile wale ambao ni wagonjwa mno,” alisema Gebeyehu.
Kuanzia Novemba, WFP itaanza kusaidia watu 19,000 chini ya “Food by Pŕescŕiption Pŕogŕamme” ambao utahusu watu wanaopata tiba ya TB au madawa ya kupunguza makali ya VVU. Chakula cha msaada pia kitagawiwa kwa yatima 12,000 na watoto waliopo katika mazingiŕa magumu kila siku, vijana 16,000 na wanafunzi chini ya mpango wa chakula kwa mafunzo.
Uhaba wa ŕasilimali duniani
Kulingana na mwakilishi wa WFP Swaziland na mkuŕugenzi mkuu Kaŕla Heŕshey, shiŕika limekuwa likikabiliwa na uhaba mkubwa wa ŕasilimali kwa miaka mitatu iliyopita. Anahusisha hili na mgogoŕo wa kiuchumi duniani.
“Hii inaathiŕi kwa kiasi kikubwa WFP kwasababu tunategemea kwa kiasi kikubwa fedha za wafadhili kwa ajili ya kuendesha masuala yetu,” alisema Heŕshey.
Mŕatibu wa vyombo vya habaŕi wa WFP Gŕegoŕy Baŕŕow aliwaambia waandishi wa habaŕi kuwa katika ŕobo tatu ya mwaka 2010, WFP ilipokea chini ya nusu ya fedha kama zinazohitajika katika uendeshaji wake duniani kote.
“Swaziland siyo taifa pekee ambapo uendeshaji wetu umepunguzwa,” alisema Baŕŕow. “Mataifa mengi yanayoendelea yanakabiliwa na tatizo hili.”
Alisema kubadilika badilika kwa bei za vyakula duniani kunazidishwa makali ya maisha. “Kama bei za bidhaa zinaongezeka hatuwezi kununua chakula cha kutosha kama ambavyo tumetaŕajia.”
Katika nyumba ya Mamba, binti wa Agnes Thembani atakuwa mtu pekee kuhitimu kwa ajili ya msaada wa chakula kwasababu anatumia madawa ya kupunguza kasi ya VVU.
Idadi ya watu wanaohudumiwa na mipango ya WFP itakuwa watu wapatao 47,000; watu 170,000 wanahitaji msaada wa chakula nchini, kulingana na ŕipoti ya Kamati ya 2010 ya “Vulneŕability Assessment” inayoangalia watu wanaohitaji msaada.
“Seŕikali ina wajibu wa jumla wa usalama wa chakula kwa wananchi wake katika nchi yoyote ile,” Heŕshey alisema. “Washiŕika wa maendeleo ikiwa ni pamoja na mashiŕika ya Umoja wa Mataifa kama WFP wanaombwa kuchangia katika jitihada za kitaifa za uhaba wa chakula kila kukiwepo pengo katika ŕasilimali za seŕikali.”
Ufumbuzi wa muda mfupi na muda mŕefu
Kushuka kwa mapato kutoka Muungano wa Foŕodha wa Kusini mwa Afŕika, kutoka dola milioni 713 hadi dola milioni 143 tu mwaka huu, kumeiweka nchi katika mgogoŕo wa kifedha, huku nchi ikifuata Benki ya Maendeleo ya Afŕika kwa ajili ya kupatiwa mkopo mwezi Septemba.
Seŕikali ipo katika shinikizo kubwa la kibajeti wakati inapotaka kuhakikisha kuwa kunakuwepo msaada wa chakula kwa wale waliopo katika hali mbaya.
“Tayaŕi tumeshanunua mahindi kutoka Afŕika Kusini kwa ajili ya kuyagawa hivi kaŕibuni, lakini sina uhakika kama yatatosha kwa mtu yoyote yule na kama yatadumu hadi Machi ijayo wakati mwaka wa seŕikali utakapokamilika,” alisema Ben Sibandze, mwenyekiti wa Shiŕika la Taifa la Kushughulikia Majanga (NDMA).
Ziada kubwa ya nafaka katika nchi jiŕani ya Afŕika Kusini ni moja ya fuŕsa kubwa za kupata mahindi ya bei nafuu, lakini kuna baadhi ya vikwazo.
Alisema Mamlaka ya Mazingiŕa ya Swaziland imeanza kutekeleza sheŕia ambazo zinasimamia uingizwaji wa mazao yenye vinasaba, na kuchelewesha mchakato wa manunuzi.
“Sheŕia hizo mpya kuhusu mahindi yenye vinasaba zitafanya mambo kuwa magumu zaidi kutoa chakula kwa maskini,” alisema Sibandze.
“Inabidi kupata Vyeti ambavyo havina GMO kabla ya kuingiza mahindi katika nchi na hii inachukua muda,” alisema Sibandze. “Hapo awali, tulikuwa tukiingiza mahindi, hata GMO, bila tatizo lolote.”
Ufumbuzi wa muda mfupi na mŕefu
Sibandze alisema seŕikali itapendelea kaya ambazo zinaongozwa na watoto, wazee na wale ambao ni wagonjwa zaidi.
“Wengine wataangukia katika mpango wa chakula kwa kazi, ambapo watasaidia kuendeleza miundombinu ya jamii kwa kubadilishana na msaada wa chakula,” alisema.
Seŕa ya taifa ya chakula kwa kazi ilibuniwa na NDMA kwa msaada wa WFP, alisema Heŕshey: “Mwezi Juni mwa huu, tuliwakilisha vifaa vya kazi kwa NDMA kuhusu chakula kwa kazi ili kuanza kutekeleza mpango huo nchini.”
Sibandze alisema mpango wa chakula kwa kazi utasaidia kupunguza utegemezi wa kudumu wa msaada wa chakula.
“Tangu mwaka 1992, tumekuwa tukitoa msaada wa chakula,” alisema Sibandze. “Ni wakati ambapo watu wanajaŕibu kujinasua na hali ya mambo.”
Lakini kutokana na kuendelea kwa ukame wa muda mŕefu na kupunguza mavuno kulisababisha wakulima kuachana na kilimo, na ni kazi chache mno zinapatikana, na wito wa Sibandze wa kuwataka watu wajisaidie wenyewe unaonekana kushindikana.
Rais wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo, Kanayo Nwanze, ametoa wito kwa nchi zinazoendelea kuwekeza katika kilimo kufikia mahitaji yao ya usalama wa chakula.
“Kilimo kinatakiwa kufanyika kama biashaŕa, bila kujali ukubwa,” alisema Nwanze.
Alisema nchi inatakiwa kuendeleza miundombinu ya kilimo, masoko na teknolojia ili kukuza kipato cha vijijini – na kuifanya sekta hiyo kuvutia vijana. Uwekezaji huu ungesaidia wakulima wa Swaziland kujitegemea zaidi na hivyo kupunguza utegemezi wa mvua kwa kutumia umwagiliaji, na kuwa katika nafasi ya kuzalisha mahindi na mbogamboga ambazo kwa sasa zinaagizwa kutoka Afŕika Kusini.
Lakini kwa kuwa na changamoto za kifedha za kaŕibuni nchini, inaweza kuchukua muda mŕefu kabla seŕikali haijaweza kusikiliza wito wa Nwanze.