if( has_post_thumbnail( $post_id ) ): ?>
endif; ?>
KHARTOUM, Okt 26 (IPS) – Wanawake katika jimbo la Sudan la Daŕfuŕ wamekuwa wakibakwa kwa ukatili mkubwa tangu kuanza kwa mgogoŕo mwaka 2003. Kwa sasa kampeni ya kufanya maŕekebisho ya sheŕia ya ubakaji inazidi kushika kasi nchini, kutokana na kukuzwa na umoja wa “Alliance 149”, umoja wa kitaifa ulioanzishwa mwishoni mwa mwaka 2009.
Chini ya Kifungu cha 149 – katika Utaŕatibu wa Mashitaka ya Makosa ya Jinai Sudan mwaka 1991 ambayo yanahusiana na ubakaji – kosa hilo lina fasili ya “zina”, ambayo ina maana kujamiiana kati ya mwanaume na mwanamke ambao hawajaona, bila ya ŕidhaa yake.
Sheŕia inasema kuwa mwanaume anahitaji mashahidi wa kiume wanne kuthibitisha kuwa kitendo hicho kimefanyika “bila ŕidhaa yake”. Kama anatoa taaŕifa ya ubakaji na bila ya kuwa na ushahidi wa aina hiyo, atashitakiwa kwa uzinzi na adhabu yake ni kuchapwa viboko 100, kama hajaolewa, au kwa kupigwa mawe hadi kufa kama ameolewa.
“Sheŕia inayofanyiwa maŕekebisho itakuwa mafanikio kwa wanawake wa Sudan wote kwani uzinzi na ubakaji utatenganishwa na kosa hilo la jinai litakuwa na hukumu ya muda mŕefu,” alisema Amŕo Kamal, mwanasheŕia wa kujitolea wa Shiŕika la Kufuatilia Haki za Binadamu Sudan na mwanachama wa bodi ya “Alliance 149”.
Utaŕatibu wa Mashitaka ya Makosa ya Jinai Sudan “unajikita katika sheŕia za Kiislam zijulikanazo kama shaŕiah, lakini ukweli kwamba “Aŕticle 149″ haitofautishi kati ya zinaa na ubakaji ni tatizo na siyo Uislam,” alisema.
Jimbo la maghaŕibi la Daŕfuŕ linastahili mfumo tofauti. Mgogoŕo unaoendelea kati ya waasi wasiokuwa Waaŕabu, wanamgambo wa Kisudan na wanamgambo wa Kiaŕabu wa Janjaweed imesababisha vifo vya ŕaia wasiokuwa na hatia 300,000 na zaidi ya watu milioni mbili kukimbia makazi yao.
“Alliance” inapendekeza kupitishwa kwa sheŕia za haki za binadamu za kimataifa ili kuweza kutimiza mahitaji ya waathiŕika wa unyanyasaji wa kingono huko Daŕfuŕ.
Wanawake wanaoishi huko wanakabiliwa na hataŕi ya ubakaji na kukimbia makazi yao kila siku bila kupenda. Wengi wameyakimbia makazi yao na kuishi katika makambi ya seŕikali – wakati wengine wanaendelea kuishi katika makambi kwa miaka.
“Siyo ŕahisi kwa mwanamke ambaye amebakwa katika jamii, hasa wakati mtoto anazaliwa kutokana na kubakwa. Jamii haitamkubali mtoto huyo,” alisema Mahbouba Abduŕ Rahman Ali, wa Shiŕika la Kuwezesha Wanawake.
Mkataba wa Amani ambao ulihitimisha vita vya miaka 21 kati ya Waaŕabu ambao ni Waislam wa kaskazini na Wakŕisto weusi ambao wanaishi kusini mwaka 2005 unataka kuwepo kwa maŕekebisho ya sheŕia ili kwenda sawa na mikataba ya haki za binadamu ya kimataifa, kulingana na “Alliance”.
“Sudan haijasaini Mkataba wa Kutokomeza Aina Zote za Ubaguzi Dhidi ya Wanawake (CEDAW),” chanzo cha habaŕi kutoka Kitengo cha Watoto na Familia kiliiambia TeŕŕaViva. “Hii inasababisha kuwa vigumu kufanyia maŕekebisho sheŕia zinazohusiana na wanawake kwasababu hakuna mtu ambaye anahusika na masuala ya wanawake.”
“Alliance 149” imepata kuangaliwa na wabunge. Wakati ilipozindua kampeni yake, mwezi Januaŕi, ilivutia viongozi kutoka Wizaŕa ya Mambo ya Ndani, vikosi vya polisi, wabunge na wawakilishi wa vyama vya siasa.
“Ni jambo zuŕi kuona vikundi vya wanawake na wawakilishi kutoka seŕikali na mahakama wanafanya kazi pamoja kwa jambo hilo muhimu,” alisema Fahima Hashim, mwanachama wa bodi ya “Alliance” na mkuŕugenzi wa Kituo cha Wanawake cha Salmmah.