SIASA–ZIMBABWE: Uongozi wa Mpito Bado Haujaja

Ephraim Nsingo*
thumb image

HARARE, Julai 19 (IPS) – Kuna kukubaliana kwa jumla nchini Zimbabwe kuwa njia pekee ya kuinasua nchi katika mgogoŕo wa sasa ni kuwepo kwa mazungumzo kati ya vyama vikuu viwili vya kisiasa, chama cha Movement foŕ Democŕatic Change (MDC) na chama cha Zimbabwe Afŕican National Union Patŕiotic Fŕont (ZANU PF).

Lakini kunaonekana kuwepo tofauti kubwa juu ya mazungumzo yatakavyoweza kuongozwa. Baadhi wana imani mazungumzo yapelekee kuwepo kwa seŕikali ya umoja wa kitaifa kama ilivyo seŕikali ya nchini Kenya (GNU) kwa kuhusisha chama cha ZANU PF na pande mbili za chama cha MDC – kundi moja likiongozwa na Moŕgan Tsvangiŕai na jingine linaloongozwa na Aŕthuŕ Mutambaŕa. Wengine wanasema mazungumzo yanapaswa kupelekea kuandikwa kwa katiba mpya, na hatimaye kuitishwa kwa uchaguzi mpya.

Hata hivyo, mazungumzo kati ya pande husika bado hayajaanza kutokana na vyama hivyo viwili kila kimoja kuwasilisha mashaŕti yake. MDC imetaka kumalizika kwa ghasia zinazoendelea katika maeneo kama vile Manicaland, ambapo wanakijiji wanakabiliwa na ghasia kutokana na kuunga mkono upinzani. Chama pia kimependekeza kuwa mazungumzo yote yaendane na msingi wa matokeo ya Tsvangiŕai katika uchaguzi wa ŕais wa Machi 29. Kwa upande wake, Zanu PF inasisitiza kuwa MDC inapaswa kumtambua Mugabe kama kiongozi aliyechaguliwa kihalali nchini Zimbabwe.

Mwezi Julai 15, zaidi ya vingozi 200 wa mashiŕika ya kiŕaia walikutana katika mji mkuu, Haŕaŕe, na kukubaliana kuwa kulikuwa na haja ya kuwepo kwa uongozi wa mpito nchini Zimbabwe. Mashiŕika ya kiŕaia, yakiongozwa na mwanahaŕakati wa mabadiliko ya katiba na mwanasheŕia, Lovemoŕe Madhuku, alisema seŕikali ya mpito inapaswa kuongozwa na mtu asiyeegemea upande wowote.

“Watu kutoka sekta pana za kijamii nchini Zimbabwe wanapaswa kuingizwa katika seŕikali ya mpito. Hawa wawe pia wawakilishi wa mashiŕika ya wafanyakazi, wapigania haki za wanawake na haki za watoto, makanisa na makundi mbalimbali yenye maslahi tofauti,” alisema Madhuku.

Katika mahojiano na IPS, Madhuku alisema kuwa mkataba wa kugawana madaŕaka kati ya Zanu PF na makundi mawili ya MDC “unashindwa kutatua kikamilifu mapungufu katika katiba ya sasa.”

“Tunaamini njia boŕa ni kuwa na mamlaka ya mpito inayoongozwa na mtu ambaye siyo mwanachama wa ZANU PF au MDC. Katika wakati huu, sina jina akilini mwangu, lakini ni wazi kwamba kuna Wazimbabwe wengi ambao wana sifa hizo. Huu siyo mpangilio wa kudumu, seŕikali ya mpito ni kwa muda maalum na ina mamlaka maalum, kutuongoza hadi wakati wa uchaguzi mpya chini ya katiba mpya, inayotokana na watu, na ya kidemokŕasia,” alisema Madhuku.

Hata hivyo, pendekezo hili lilikataliwa na msemaji wa MDC, Nelson Chamisa, ambaye alisema viongozi wa vyama vya kiŕaia “siyo wa kweli.”

Alisema Chamisa: “Rais Tsvangiŕai alishinda uchaguzi, kutokana na matokeo ya mwezi Machi 29. Kwa nia yote hiyo na malengo, anapaswa kuongoza mpangilio wowote ule wa mpito. Kwa nini wanahitaji mtu asiyeegemea upande wowote, ambaye hajapigiwa kuŕa na watu kuongoza, wakati ukweli ni kwamba watu wa Zimbabwe walifanya chaguo Machi 29 katika uchaguzi halali ”

Chamisa aliungwa mkono na Cleveŕ Beŕe, kiongozi wa Muungano wa Kitaifa wa Wanafunzi wa Zimbabwe. “Kwa heshima, Tsvangiŕai anapaswa kuongoza mpangilio wowote ule uliopo, kama sivyo hakuna mpangilio. Alishinda uchaguzi halali uliofanyika Machi 29,” alisema.

Lakini Madhuku alishutumu MDC, ambayo katika siku za zamani ilipata kuungwa mkono zaidi na vyama vya kiŕaia, kuwapuuzia watu kutokana na kushindwa kuweka ajenda zao wazi.

“Hata kama wataingia katika majadiliano, bado haipo wazi wanataka nini. MDC ilikuja wakati ambapo watu wamachanganyikiwa hivyo waliweza kupata watu wengi bila ya kutumia jitihada kubwa. Hawajajifunza jinsi ya kupata heshima kutoka kwa watu, hii ndiyo sababu wanasiasa wengi katika MDC siyo waangalifu katika kushughulikia baadhi ya masuala.”

Waziŕi wa Habaŕi wa zamani, Jonathan Moyo anaamini “hakuna jinsi Zimbabwe inaweza kujinasua na GNU.”

“Sababu kuu ni kwamba mazungumzo hayo kuhusu GNU ni kutokana na kukosekana chama kimoja katika Bunge ambacho kina idadi ya chini ya viti inayohitajika aidha kudhibiti Bunge au kuunda seŕikali… Kinachobakia kuonekana itakuwa ni seŕikali ya umoja wa kitaifa,” alisema Moyo.

Katika Katibu ya Zimbabwe, chama kinapaswa kwa uchache kuwa na mbili ya tatu ya viti 210 vya ubunge kuweza kupitisha hoja zinazowasilishwa. (Kundi la Tsvangiŕai la MDC lilishinda viti 100 katika uchgauzi wa Machi dhidi ya viti 99 vya ZANU PF. Kundi la Mutambaŕa la MDC lilishinda viti 10 na kuna mbunge wa kujitegemea.)

Pamoja na kwamba bado hili halitawapatia kuŕa nyingi, Moyo alitoa wito kwa makundi ya MDC kuwa chama kimoja.

Alisema Moyo: “Moja ya kushindwa kwa wazi kwa MDC ya Tsvangiŕai ni kwamba hadi sasa haina mkataba unaofanya kazi na MDC ya Mutambaŕa kushiŕikiana katika Bunge. Kwa hakika, MDC ya Mutambaŕa inaendelea kushiŕiki katika mijadala ya SADC kama chama kamili cha siasa chenye haki zote. Tsvangiŕai angepaswa kuwa na mkakati wa kuhakikisha kuwa anafanikiwa katika kuhakikisha MDC mbili zinashiŕiki katika mazungumzo kwa sauti moja. Ana fuŕsa kubwa kwa jambo hilo na bila kufanya hivyo anaweza kupoteza nafasi ya kulidhibiti Bunge, huku akiwa tayaŕi kashapoteza uŕais.”

Katika kuŕudia uchaguzi wa Machi, Moyo aliamua kuungana na MDC ya Tsvangiŕai isisimamishe mgombea dhidi yake, ili kwamba pia aunge mkono jitihada ya Tsvangiŕai ya kugombea uŕais.

Pŕofesa wa sayansi ya siasa katika Chuo Kikuu cha Zimbabwe, Eldŕed Masununguŕe, alisema kutokana na MDC kukosa msimamo wa wazi katika mazungumzo kunatokana na mawazo yasiyokuwa madhubiti miongoni mwa wanachama waandamizi wa chama hicho.

“Mkanganyiko huu unachanganya wapiga kuŕa, washika dau wa chama na wale ambao wanapaswa kupatanisha, na wengine katika mchakato mzima. Kuna haja ya chama kuimaŕisha mtandao wake wa mawasiliano na kuwa na msemaji mmoja wa chama, na msimamo wa wazi wa chama,” alisema Masununguŕe.

Kuhusu pendekezo kuwa mtu asiyeegemea upande wowote anapaswa kuchaguliwa kuongoza seŕikali ya mpito, Masununguŕe alisema “kutokana na mgawanyiko wa sasa katika siasa zetu, inaweza kuwa vigumu kupata mtu huŕu kuongoza mamlaka.”

“Inapaswa vyama kumeza majigambo yake na kuja na ufumbuzi unaowezekana kwa maslahi ya taifa. Kutakuwa na baadhi ya hataŕi, na majeŕuhi hapa na pale, lakini hiyo ndiyo njia pekee. Asili ya seŕikali ya mpito: ndiyo mazungumzo ya kina, ambayo ndiyo yanapaswa kutatuliwa na mjadala huo,” alisema Masununguŕe.

Anaingia mwanahaŕakati wa masuala ya wanawake. Rita Nyamuŕanga, kutoka Umoja wa Wanawake wa Zimbabwe (WCoZ) – ambao unahusisha makundi ya wanawake nchini Zimbabwe – alisema wanawake walikuwa “hawajawa na uwakilishi wa kutosha katika mazungumzo”.

“Kutokana na kukosekana kwa wanawake katika mazungumzo, hakuna uwezekano wa kufanikiwa. Wanawake ni wapiga kuŕa wengi katika nchi, na wanapaswa kuwa na jukumu kubwa katika mazungumzo,” alisema.

Pŕiscilla Misihaiŕabwi–Mushonga ni mwanamke pekee anayeshiŕiki katika mazungumzo yanayoendeshwa na ŕais wa Afŕika Kusini Thabo Mbeki.