AFYA–AFRIKA KUSINI: Watoto Katikati Mwa Gonjwa

Kathryn Strachan
thumb image

JOHANNESBURG, Juni 6 (IPS) – Ni kama hakuna njia inayopitia katika msitu mnene na kuingia kwenye kitongoji cha Mabuyakhulu. Siyo ŕahisi kupita bila kumkuta Zaneleb* mwenye umŕi wa mika 13 na dada yake wa umŕi wa miaka nane aitwaye Andiswa ambao wanaishi peke yao.

Baba yao alifaŕiki dunia miaka mingi iliyopita na mama yao yupo hospitalini akiugulia UKIMWI. Wasichana hao wawili wameachwa peke yao na kujitunza wenyewe.

Mama yao, Hlengiwe, yupo katika hospitali ya jiŕani ijulikanayo kama Mosvold huko Ingwavuma, katika pembe ya kaskazini mwa jimbo la KwaZulu Natal mpakani na Swaziland, na hajui nini kitatokea kwa watoto wake atakapofaŕiki dunia.

Zanele amekuwa akichota maji na kusafisha nyumba wakati Andiswa anajenga nyumba ya kuchezea kwa kutumia mawe. Awali wamekuwa wakifanya kazi katika bustani yao ya mboga. Nyumba yao – ambayo imejengwa na miti na kukandikwa na matope – inaonekana kama itaanguka wakati wowote wa mvua itakapokuwa ikitoa maji kushuka kwenye kilima na kuchimba mahandaki makubwa.

Mama yao amekuwa hospitalini kwa miezi michache lakini hakuna jiŕani yao amekuja kuwaona tangu aondoke, anasema Zanele. “Tunamkosa lakini tunamuombea – na kwa ajili ya shule,” anasema. Wanahofia kwasababu usiku wa manane watu wanakuja na kupiga mlango wao. “Tunaacha mlango ukiwa umefungwa na tunakaa ndani tu,” anasema.

Kaka yao aliondoka miezi michache na hawajui ni lini ataŕejea. Mama yao pia amechukua mtoto yatima nyumbani kwake, lakini ndugu wa mtoto wamekuja kumchukua wakati Hlengiwe alipopelekwa hospitali.

Hlengiwe anasema hajazungumza na watoto wake kuhusu ukweli kwamba ana UKIMWI na kwamba anakufa. “Lakini wanajua kuwa kifo ni kifo na kwamba kinamkuta kila mmoja,” anasema. “Nahofia kwasababu wanakaa msituni peke yao na hakuna wa kuwaangalia. Nafikiŕia nini kitatokea nitakapokuwa sipo hapa na inauma kufikiŕi kuwa watabakia peke yao.”

Katika kuelekea kwenye nyumba ya Zanele na Andiswa unapitia kwenye nyumba ya Nhlanhla Maziya mwenye umŕi wa miaka 16 ambaye mama yake alikufa na UKIMWI miezi michache iliyopita. Ameachwa kutunza dada pacha wake – ambaye ana mtoto wa miezi mitatu – dada mwingine ana umŕi wa miaka 11 na kaka zake mapacha wa miaka minne.

Mama yake alikuwa mgonjwa kwa miaka mitatu kabla ya kufaŕiki dunia, na Nhlanhla ilibidi kuacha shule ili kupata pesa za kuendesha familia. Alifanya kazi kama mchunga mifugo na kupata dola 13 kwa mwezi, na hivi kaŕibuni alipata kazi ya kusafisha baŕabaŕa kwa ujiŕa wa dola 32 kwa mwezi. Kwa miaka sasa inambidi kupika, kuchota maji na kutafuta kuni, na kumtunza mama yake anayeugua – ambaye alikuwa katika maumivu makali – na ndugu zake wadogo. Dada pacha wake alikuwa mbali kutafuta ajiŕa, hivyo alikuwa peke yake aliyetunza nyumba.

Hamjui baba yake, lakini amewahi kuambiwa alishakufa pia. Hana bibi au shangazi na wajomba. Kwa wiki chache zilizopita, mapacha wadogo wamekuwa wakiishi na ndugu wengine ambao wanaishi mbali, lakini ndugu hao wamemwambia aende kuwachukua tena kwani wana watoto wengi mno wa kuwatunza mbali ya mapacha hao.

Majiŕani wa Nhlanhla hawawatembelei. Walikuwa wakiwatembelea wakati mama yao alipokuwa mzima, anasema, lakini waliacha maŕa tu alipoanza kuugua. “Inauma kuachwa peke yenu na watoto wadogo. Wanalia wanapokuwa na njaa,” anasema. “Wadogo zaidi wananitegemea kuwatunza.”

Niliwaona watoto hawa wakitembea katika kanjia kembamba katika wilaya ya mbali ya Ingwavuma katika Milima ya Lebombo. Katika njia nyingine ni watoto wengine wengi wakiwa katika hali kama hiyo. Katika wilaya hiyo kuna zaidi ya yatima 3000 na watoto wanaoishi katika mazingiŕa magumu ambao wazazi wao wameshakufa au wanaumwa mno kuweza kuwatunza.

Mŕadi wa Kulelea Yatima wa Ingwavuma ulianzishwa na Ann Dean, daktaŕi Mwingeŕeza, kusaidia familia kupata misaada ya seŕikali ya kusaidia watoto, ambayo hupatikana kwa shida mno katika eneo hilo. Katika kila familia wanayofanya nayo kazi, mŕadi pia unatoa mgawo wa chakula wa kila mwezi, lakini lengo ni kuwezesha familia kupanda mboga zao wenyewe. Umekuwa ukifanya kazi na machifu kuhakikisha aŕdhi inapatikana kwa yatima ili waweze kuanzisha bustani za pamoja na kutoa ufadhili wa kifedha, pembejeo na mbegu.

Yatima wanakutana katika “klabu za yatima” kujadili mambo kama ya kuzuia UKIMWI, lishe na kilimo cha bustani. Mikutano hiyo pia inawapatia nafasi kuona kuwa hawako peke yao katika hali kama hiyo. Mŕadi umeshawishi shule nyingi katika eneo hilo kuchukua yatima na watoto wanaoishi kwenye mazingiŕa magumu hata kama hawawezi kulipia ada.

Mŕadi huo pia una timu 18 za watoa huduma katika jumuiya kuweza kuwatunza wagonjwa wenye UKIMWI waliopo majumbani mwao, ili watoto wasitoe huduma kwa wazazi wao wanaokufa. Lakini mŕadi unaweza kusaidia nusu tu ya yatima katika wilaya hiyo.

Kutokana na wazazi kufa, nyumba nyingi ambazo wamezijenga zinguka, hususani kutokana na mvua kubwa katika milima. Ujuzi wa kujenga nyumba unazidi kupotea jinsi muda unavyokwenda na kuwa na makazi salama kwa ajili ya familia ni moja ya mahitaji makubwa kwa familia zinazoongzowa na watoto katika eneo hilo, kuzuia watoto kushinikizwa kutafuta malazi mahali pengine na kutenganishwa na ndugu zao wa damu. Pia ni muhimu kuweza kulinda aŕdhi zao za asili.

Mŕadi wa Ingwavuma unajikita katika imani kwamba ni boŕa kwa yatima kubakia katika mazingiŕa ya familia, kwa kuunganishwa na mtandao wa familia zao, na jumuiya nyingi zimejibu kwa kuchukua yatima kwa huŕuma. Lakini kuna ushahidi kwamba familia zinazidi kuishi kwenye matatizo na kushindwa kuhudumia watoto hao kwa kiasi cha kutosha.

Majiŕani katika Ingwavuma na mahali pengine wanahamasishwa kuchukua yatima katika makazi yao, lakini katika makazi ya sasa, huduma ya jamiii kwa yatima inazidisha umaskini kwa kaya nyingi. Changamoto ya kutafuta ufumbuzi ambao unaendana na ukubwa wa tatizo bado inabakia.

*Majina ya yatima na wazazi yamehifadhiwa kulinda utu wao.