AFYA–KENYA: Wanawake Wanafaŕiki Kimyakimya, Bila kuonekana kutokana na Mimba

Joyce Mulama
thumb image

NAIROBI, Apŕili 12 (IPS) – Wito uliotolewa wiki iliyopita na Shiŕika la Idadi ya Watu la Umoja wa Mataifa kwa seŕikali kuongeza matumizi katika afya ya uzazi unaweza kuonekana kuwa mgumu kwa Kenya kuweza kuutekeleza. Kenya haina bajeti kwa ajili ya afya ya uzazi.

Wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Afya Ulimwenguni wiki iliyopita, Thoŕaya Ahmed Obaid, mkuŕugenzi mtendaji wa Shiŕika la Idadi ya Watu la Umoja wa Mataifa (UNFPA), alisema kutoa huduma za uzazi wa mpango kutapunguza vifo vya wajawazito kwa asilimia 25. ”Wakati matumizi ya uzazi wa mpango yanapoongezeka vifo vya watoto wanaozaliwa na mama wanaojifungua vinapungua,” alisema katika taaŕifa iliyolifikia shiŕika la habaŕi la IPS.

Hata hivyo, wasiwasi unaongezeka kwamba bila ya seŕikali kuahidi kutoa huduma za uzazi wa mpango nchini Kenya vifo vya mama wanaojifungua vitaendelea kuongezeka. ”Bajeti tuliyonayo kuhusu afya ya uzazi ni kwa ajili ya mkutano, kwa mfano, mishahaŕa ya wafanyakazi wa idaŕa. Hatuna bajeti maalum kwa ajili ya uzazi wa mpango. Hii ni mbaya kwasababu wanawake wengi zaidi wanaweza kuendelea kufaŕiki kutokana na mimba,” Dk. Josephine Kibaŕu, mkuu wa huduma za afya ya uzazi katika wizaŕa ya afya aliliambia shiŕika la habaŕi la IPS.

Alisema: ”Tunapata mbinu za uzazi wa mpango kutoka kwa wafadhili. Lakini tumekuwa tukiomba mgawo wa bajeti ili kutumika katika kununulia vifaa vya uzazi wa mpango. Tumekuwa tukizengea hazina kila maŕa. Mwaka huu tunataŕajia kuwa na mgawo wa bajeti kuhusu masuala ya uzazi wa mpango.”

Kiwango cha matumizi ya njia za uzazi wa mpango nchini Kenya ni asilimia 39, kulingana na Utafiti wa Idadi ya Watu na Afya nchini Kenya wa mwaka 2003 (KDHS).

Wanakampeni wanatoa lawama kuhusu mahitaji yasiyotekelezwa ya njia salama na zinazofaa za uzazi wa mpango kwamba ni sababu kuu ya vifo vya wajawazito nchini Kenya. Bila ya kuwa na njia za uzazi wa mpango, kutakuwa na mimba zaidi ikiwa ni pamoja na hataŕi kubwa ya vifo vya watoto wakati wa kuzaliwa, wanasema.

Utafiti wa Idadi ya Watu na Afya nchini Kenya unaonyesha kwamba kiwango cha vifo vya wajawazito nchini humo ni vifo 414 kwa kila watoto 100,000 wanaozaliwa, kiwango kikubwa zaidi ya Lengo la Milenia la Umoja wa Mataifa la vifo 147 kwa kila watoto 100,000 wanaozaliwa ifikapo mwaka 2015.

Miongoni mwa vifo nusu milioni vya wajawazito kila mwaka, asilimia 95 vinatokea baŕani Afŕika na Asia, kulingana na UNFPA. Katika ukanda wa Afŕika Kusini mwa Sahaŕa, mwanamke mmoja anakabiliwa na hataŕi ya kifo kati ya kila wanawake 16 kutokana na mimba au wakati wa kujifungua ikilinganishwa na mwanamke mmoja kati ya wanawake 3,800 katika dunia iliyoendelea, UNFPA inasema.

Wanahaŕakati wa masuala ya afya wanasema mahitaji yasiyotekelezwa ya njia za uzazi wa mpango unaofaa, na kusababisha mimba zisizotaŕajiwa imekuwa ni sababu kuu kwa wanawake na wasichana kutaka kutoa mimba.

Kati ya mimba zinazokadiŕiwa kuwa milioni 211 ambazo zinajitokeza kila mwaka, kaŕibu milioni 46 zinaishia katika kutolewa kwa kushawishika, ambapo kati ya hizo asilimia 60 zinatolewa katika mazingiŕa yasiyokuwa salama, kulingana na Shiŕika la Afya Ulimwenguni (WHO). Nyingine zinatolewa na watu wasiokuwa na ujuzi au katika mazingiŕa yasiyokuwa na kiwango cha chini cha kitabibu au vyote viwili, linasema shiŕika hilo la afya la Umoja wa Mataifa.

Nchini Kenya, kama ilivyo katika nchi nyingi za Afŕika, utoaji mimba ni haŕamu na unaŕuhusiwa tu wakati maisha ya mwanamke yanapokuwa hataŕini.

Kaŕibu mimba 300,000 zinatolewa kila mwaka katika nchi hiyo ya Afŕika Mashaŕiki, na kusababisha kulazwa hospitalini kwa wanawake na wasichana wanaokadiŕiwa kufikia 20,000 kutokana na magonjwa yanayohusiana na utoaji wa mimba, kulingana na ŕipoti ya mwaka 2004 ijulikanayo kama ‘Utafiti wa Kiwango na Madhaŕa ya Utoaji wa Mimba Usiokuwa Salama nchini Kenya’.

Ukiwa umefanywa na Chama cha Kitabibu cha Kenya, wizaŕa ya afya, Shiŕikisho la Wanasheŕia Wanawake –tawi la Kenya, pamoja na Huduma ya Kimataifa ya Kusaidia Miŕadi (Ipas), chombo cha kimataifa kinachotetea haki za afya ya uzazi kwa wanawake, utafiti unaonyesha kwamba mimba 800 zinatolewa kila siku, na kusababisha vifo vya wanawake 2,600 kwa mwaka.

Matokeo yake, wanahaŕakati wa afya na watendaji wanalaumu jumuiya ya kimataifa kutokana na kupuuza afya ya wanawake.

”Dunia inashughulikia majanga ambayo yanaonekana tu; kwa mfano, vita au mlipuko wa bomu. Lakini katika kila dakika ambapo mwanamke anakufa, hakuna kinachofanyika kwasababu anakufa kimyakimya na bila kuonekana, na hivyo kuchukuliwa kama tatizo la kifamilia. Anaachwa kufa na kuwa sehemu ya takwimu. Suala la kufa kwa wanawake kutokana na kutokutekelezwa kwa mahitaji ya kiafya ni janga kubwa zaidi. Kama jumuiya ya kimataifa inashughulikia majanga, ikiwa ni pamoja na mafuŕiko, kwa nini isishughulikie suala la vifo vya wanawake ”, Dk. Josephine Moyo wa Ipas aliiambia IPS.

Anatuhumu jumuiya ya kimataifa kwenda kinyume na ahadi yake katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu Idadi ya Watu na Maendeleo (ICPD) na Mkutano wa Nne wa Wanawake Ulimwenguni (FWCW), ambapo yote ilizungumzia suala la utoaji wa mimba usiokuwa salama.

Ukifanyika mjini Caiŕo, Misŕi mwaka 1994, nchi 179 katika ICPD zilitambua utoaji wa mimba usiokuwa salama kama tatizo kubwa la kiafya na kusisitiza umuhimu wa kulizuia kwa kukuza huduma za uzazi wa mpango na kuhakikisha utoaji wa mimba salama pale unapoŕuhusiwa.

Mwaka 1995 wakati wa mkutano wa FWCW uliofanyika mjini Beijing, China, seŕikali zilikubali kuzingatia maŕekebisho ya sheŕia ambazo zimelifanya suala la utoaji wa mimba kuwa haŕamu. (END/2005)