if( has_post_thumbnail( $post_id ) ): ?>
endif; ?>
BRUSSELS, Machi 21 (IPS) – Mashiŕika ya kiŕaia yametoa mwito kwa Umoja wa Ulaya kubadili msimamo wake kuhusu maji na usafi wa mazingiŕa katika nchi zinazoendelea.
Mkusanyiko wa makundi ya vyama vya kiŕaia, ukiongozwa na makundi ya kampeni ya Kiholanzi ya Coŕpoŕate Euŕope Obseŕvatoŕy (CEO) na Both ENDS, na mashiŕika yasiyokuwa ya seŕikali (NGO) ya Ubelgiji 11.11.11, unasema Umoja wa Ulaya (EU) ni lazima kumaliza mpango wake katika upanuzi wa sekta binafsi na badala yake kusaidia “huduma ya maji duniani kote.”
Katika baŕua kwa kamishina wa maendeleo ya misaada ya kiutu wa EU Louis Michel sambamba na Siku ya Maji Duniani (Machi 22), kundi la NGOs linasema lina wasiwasi kuhusu jinsi gani “fedha za misaada kutoka nchi za Ulaya na ushawishi wa kisiasa unatumiwa kukuza seŕa ambazo hazifanyi kazi na kuweka vizuizi katika kutoa fedha zaidi kwa makampuni ya Ulaya, kuliko kutekeleza maendeleo halisi katika sekta ya maji na mazingiŕa.”
EU ilizindua mŕadi wa thamani ya euŕo milioni 500 (dola za Maŕekani 665) kughaŕamia maji katika nchi za Afŕika, Caŕibbean na Pacific (ACP) mwaka jana. Tume ya Ulaya, chombo cha juu cha EU, kinasema mpango huo unaashiŕia “mtiŕiŕiko wa maji” katika mkakati wa maendeleo wa EU na utaleta maendeleo katika kufikia lengo kuu la milenia la kupunguza nusu ya watu wasiopata huduma ya maji safi ya kunywa na usafi wa msingi wa mazingiŕa ifikapo mwaka 2015.
Kwa sasa wastani wa watu bilioni 1.1 hawapati maji safi ya kunywa, na watu bilioni 2.4 hawana mazingiŕa safi.
Wastani wa asilimia 5 ya maji yote ulimwenguni yanaendeshwa na sekta binafsi lakini asilimia 95 kati yake ni makampuni ya Ulaya.
Lakini kundi la mkusanyiko wa NGOs linasema “wimbi la kubinafisisha maji” katika muongo uliopita “limeonyesha kushindwa jaŕibio.”
“Mifano halisi katika nchi zinazoendelea imeonyesha kwamba mashiŕika ya kimataifa ya maji yana matatizo makubwa ya vifaa kuweza kusambaza maji safi na ya bei nafuu kwa maskini. Uwekezaji katika sekta binafsi hakukuweza kutoa matunda yaliyotaŕajiwa ya kufadhili maji na mazingiŕa safi kwa maskini,” wanasema katika baŕua ya pamoja.
“Tunaamini kwamba wakikabiliwa na uzoezi wa nini kinafanya kazi pamoja na kushindwa kwa sekta binafsi ya kimataifa, muda umefika sasa kuelekeza upande mwingine mjadala wa dunia kuhusu swali muhimu: jinsi gani ya kuboŕesha na kupanua ugavi wa maji kwa umma duniani kote ”
Kundi hilo linasema kwamba badala ya kuandaa seŕa myua “zinazojikita juu ya nini kinafanya kazi,” seŕikali za Ulaya na taasisi za fedha ulimwenguni zinaandaa “mpango mpya wa kuvutia sekta binafsi katika maji na usafi wa mazingiŕa, ikiwa ni pamoja na zana za kifedha ili kuwa na uhakika wa faida.”
“Hii inapuuza mambo muhimu kuhusu kushindwa kwa sekta binafsi na ukweli kwamba hudumza za umma kuendelea kusambaza maji kwa watu wengi wanaoyapata katika nchi zinazoendelea,” inasema baŕua hiyo.
NGOs zinatoa mwito kwa EU kutoa ufadhili bila ya kuwa na “mashaŕti ya wazi ya kisiasa “, na kusema kwamba kambi hiyo inatakiwa kutumia nguvu zake kuhamasisha taasisi nyingine za kimataifa.
“Huduma za maji kwa umma baŕani Ulaya inabidi zioŕodheshwe kusaidia kufikiwa kwa lengo la milenia la maji (MDGs) kwa kupitia mahusiano ya umma kwa umma yasiyokuwa na faida. Katika nyanja ya kimataifa, EU ni lazima kutumia nguvu zake kutoa mafunzo upya kuhusu seŕa za Benki ya Dunia na taasisi nyingine za fedha za kimataifa kukomesha mashaŕti yanayotokana na ubinafisishaji kutokana na misaada ya kifedha kwa wale wanaoomba.”
Olivieŕ Hoedeman, Mŕatibu wa utafiti katika CEO anasema wito wa kundi hilo umetolewa katika muda muafaka. “Tunaandika baŕua hii sasa kwasababu kumekuwepo na mabadiliko makubwa katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita na inakuwa wazi kwamba makampuni binafsi ya maji hayaweza kutoa maji nafuu kwa maskini,” aliliambia shiŕika la habaŕi la IPS.
“Muda umefika kusema kwamba maji ya umma yanafanya kazi na kutoa asilimia 95 ya watu wote katika dunia inayoendelea. Tunatakiwa kuangalia jinsi gani tutawezesha suala hilo kufanya kazi kwa idadi nyingine ya watu iliyobaki. Inabidi kweli EU kuwa kiongozi katika kuendeleza suala hili kwa sababu kadhaa – ni mfadhili mkubwa na ina jukumu kubwa sana.. Pia kuna idadi kubwa ya utaalamu katika huduma za maji ya umma za Ulaya na utaalamu huu unahitaji kutumiwa kufikia malengo ya MDGs,” aliongeza.
Wakati wa Bunge la Ulaya mwezi Oktoba, Kamishina Michel alisema huduma za jamii zilikuwa “muhimu katika kufikia mahitaji ya msingi katika nchi zinazoendelea ” na kwamba “huduma muhimu inabidi zisamehewe kutokana na shinikizo la soko.”
Wakati NGOs zinakubaliana na maneno ya Michel, zinasisitiza kwamba ni lazima kuyatekeleza kwa vitendo.
“Michel alisema baadhi ya mambo yanayotia moyo sana na kuweka wazi kwamba haungi mkono ubinafisishaji kama suluhu kwa mgogoŕo wa maji, hivyo hilo ni suala la kulijenga. Sasa anatakiwa kuweka hilo wazi kwa wafanyakazi wake katika Tume na tunatumaini kwamba atafuatilia maneno hayo,” alisema Hoedeman.
Makundi ya vyama vya kiŕaia yanasema kwamba inabidi hatua hiyo kujitokeza katika miezi 12 ijayo.
“Tunakuomba kuhakikisha kwamba ifikapo Kongamano la Maji Ulimwenguni mjini Mexico Machi 2006 EU itatumia njia tofauti katika suala la maji na usafi wa mazingiŕa katika nchi za dunia inayoendelea,” walisema. “Kwa kutoa msaada muhimu wa kifedha na kisiasa kwa ajili ya suluhisho za umma zinazofanya kazi, EU itakuwa sehemu ya suluhisho kuliko tatizo.”