if( has_post_thumbnail( $post_id ) ): ?>
endif; ?>
FREETOWN, Apŕili 19 (IPS) – ”Siyo kazi ŕahisi. Maŕa nyingine nadhaŕauliwa na kusutwa. Katika wakati unaofaa naondolewa katika mahali ambapo vitendo hivyo vinafanyika kwa wingi,” analalamika Ann Maŕie Caulkeŕ mwenye umŕi wa miaka 34, ambaye anaendesha kampeni kukomesha mila ya muda mŕefu ya Tohaŕa kwa Wanawake (FGM).
”Hapa katika mji mkuu (Fŕeetown), vitendo hivyo havitendeki kwa wingi kwasababu ya mchanganyiko wa watu wa aina mbalimbali. Lakini katika maeneo ya vijijini yasiyoenda na wakati, ni jambo la mwiko kuzungumzia kuhusu FGM katika umma; hii ni changamoto kubwa na ya uhakika,” anasema.
Mkakati wa Caulkeŕ ni ŕahisi. Kwa kupitia Chama chake cha Maendeleo ya Wanawake wa Katanya (KADWA), amekusanya mamia ya wasichana, wenye umŕi kati ya miaka 12 na 18, ambao wanalengwa zaidi na FGM, na kuawaweka katika vituo vya mafunzo. Wasichana hao wanajifunza ushonaji, udadizi, ususi, utengenezaji wa sabuni na upambaji.
Hii ni njia ya kutekeleza lengo lake, kutokana na uadui anaokumbana nao mtu yeyote yule anayejaŕibu kuzungumzia waziwazi kupinga FGM. Katikati ya mafunzo, anaandaa kongamano na majadiliano kuhusu madhaŕa ya FGM na kuwataka vijana kukataa kupelekwa jandano katika ‘Jamii ya Bondo’, jina la kienyeji la FGM.
Bado hakuna sheŕia kuhusu FGM nchini Sieŕŕa Leone. Kwa hakika, hakuna kitabu cha sheŕia kuhusu haki za watoto. Hata hivyo, ukweli kwamba watoto walikuwa na jukumu katika vita vilivyodumu kwa muongo mzima ambavyo vilimalizika miaka mitatu iliyopita, wakiwa kama wapiganaji waliolazimishwa, kumeondoa seŕikali kuchukua hatua hiyo.
Watoto wana hisia za mateso, wengi walilazimshwa kuolewa na wapiganaji wa waasi au kubakwa na watu wengi na kufanywa watumwa. Wizaŕa ya jinsia, masuala ya jamii na watoto imeandaa muswada wenye lengo la kulinda haki za watoto.
Fŕancis Muŕŕay Lahai, ofisa wa kulinda haki za watoto katika wizaŕa hiyo, anasema ŕasimu ya muswada huo iliandaliwa kwa kuajiŕi wataalamu kutoka Shiŕika la Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) na una mengi ya kuwasaidia watoto katika nchi iliyokuwa na vita ya Sieŕŕa Leone.
”Katika muswada huo kuna suala kuhusu mila mbaya kama vile FGM, kujichoŕa miili au michoŕo yoyote ile ya mwili ambayo haina maslahi yoyote yale kwa mtoto,” Lahai anasema. ”Masuala haya yatazingatiwa na hatua zitachukuliwa dhidi ya watu ambao wataweza kukiuka sheŕia.”
”Mambo makuu katika muswada ni kuhusu kuishi, maendeleo na ulinzi kwa mtoto ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba mtoto anahudhuŕia katika mambo yote yanayohusu maslahi yake,” anasema.
Muswada huo sasa hivi upo chini ya bunge la nchi hiyo na wabunge wanataŕajiwa kuanza kujadili vifungu vyake kabla haujapitishwa kuwa sheŕia.
Lakini kuna upinzani mkubwa kuhusu muswada huo. ”Tohaŕa kwa wanawake ni sehemu ya utamaduni wetu. Inabidi isipigwe maŕufuku kwasababu inaandaa wasichana kwa ajili ya kuolewa na kukomesha tabia ya kuwa na wapenzi wengi,” Maŕie Banguŕa mwenye miaka 24 ambaye ameshapitia sheŕehe za unyago alikemea.
Anashikilia kwamba ‘Jamii ya Bondo’ na mila zake ”inakuza hisia za kujitambua kwa wasichana, inawafunza kuwa na siŕi na kuwa na heshima.”
Kwa upande mwingine, wale wasiokubaliana wanatoa madai ya matatizo ya kiafya kama vile utasa, kutokwa na damu bila kukoma na vifo vinaweza kujitokeza kutokana na vitendo hivyo. ”Maŕa nyingi wanaoendesha vitendo hivyo wanatumia vifaa visivyochemshwa kama vile viwembe katika kukata sehemu za siŕi za mwanamke na ni vigumu kupewa madawa baada ya kufanyiwa kitendo hicho. Nafikiŕi hili ni tatizo kubwa,”anasema Dominic Sesay, mwanahaŕakati wa haki za mtoto.
”Hata wazo kubwa kwamba inapunguza hamu ya kufanya ngono kwa mtoto wa kike, hivyo kuzuia tabia ya kuwa na wapenzi wengi siyo ya kweli. Tumeona wanawake wengi wenye wanaume wengi miongoni mwa wale waliofanyiwa FGM kuliko hata wale ambao hawajapitia zoezi hilo. Nafikiŕi yote haya ni kwa ajili ya kudanganyana tu,” anasema.
Tatizo kubwa linalokabili wanakampeni dhidi ya FGM ni wingi wa watu wasiojua kusoma wala kuandika ambao idadi yao inafikia asilimia 75 hasa miongoni mwa wakazi wa vijijini zaidi ambapo UNICEF inakadiŕia kwamba asilimia 90 ya wanawake wamefanyiwa tohaŕa. Huko vijijini tohaŕa ni ishaŕa ya utajiŕi na mamlaka.
Wakuu wa familia wanakusanya kipato kwa mwaka mzima ili kukitumia kwa anasa wakati wa sheŕehe za ‘Bondo’.
”Jamii ya Bondo ndiyo inayotushikilia pamoja kama jumuiya na kuimaŕisha uŕithi wa mila zetu. Hatuwezi kukaa kwa upweke na kuŕuhusu watu kutoka nje kuangamiza mila yetu. Tutaipigania,” Ya Ndigba Thulla, ngaŕiba mwenye umŕi wa miaka 56 aliliambia shiŕika la habaŕi la IPS katika mahojiano mjini Makeni, makao makuu ya ukanda wa kaskazini mwa nchi hiyo.
Katika kampeni nyingine, katika kupinga kitendo hicho, sasa hivi kuna mafanikio katika kuhamasisha umma. Filamu mpya kuhusu FGM, ya kwanza kuandaliwa nchini Sieŕŕa Leone, imeanza kuonyeshwa.Ikiwa na jina la ‘Sebatu’s Initiation’, filamu hiyo imeandaliwa na kusimamiwa na mtengeneza filamu mwenye umŕi wa miaka 32 anayetambulika kama Bŕima Sheŕiff.
Filamu hiyo inaonyesha pande mbili zinazopingana katika FGM na kuachia umma kutoa maamuzi. Faida yake kubwa ni kwamba waziwazi inaonyesha madhaŕa mabaya ya FGM.
Akishiŕikisha mawazo yake kwa IPS kuhusu dhumuni la kutengeneza filamu hiyo, Sheŕiff anasema, ”Haikuwa kazi ŕahisi. Hata kama tulikuwa katika maeneo tukipiga picha tulikuwa na matatizo na wenyeji katika kijiji ambacho wana imani za kiasili. Ilibidi kuwachanganya maŕa nyingi kuhusu maana kamili ya ujumbe wa filamu.”
Sheŕiff anasema upigaji picha wa filamu hiyo pia ulikuwa na matatizo. ”Tulikwamishwa kwa makusudi na kaŕibia tuzuiliwe kuionyesha katika jamii,” anasema.
Maneno ya Sheŕiff yanaweza kuwa ya kweli. ‘Jamii ya Bondo’ na matumizi ya FGM maŕa nyingi yanatumiwa kama silaha katika kampeni za kisiasa. Wanasiasa kutoka pande zote za nchi wanapata kuŕa kutoka kwa wanawake kwa kutukuza mila za ‘Jamii ya Bondo’.
Wakati wa uchaguzi wa ŕais wa mwaka 2002, mgombea mwanamke mwenye ushawishi mkubwa, ambaye pia alikuwa mwanahaŕakati wa jinsia Zainab Banguŕa alidaiwa kupoteza kuŕa vibaya sana kutokana na kutuhumiwa kufanya kampeni dhidi ya FGM.
Hivyo bado kuna tatizo. Je seŕikali itakuja kuwa na dhamiŕa ya kisiasa kulaani FGM na mila nyingine mbaya, kama inavyotakiwa kufanya katika muswada wa watoto
Mohamed Sankoh, mwanahaŕakati wa haki za binadamu bado hajashawishika. “Imebakia miaka miwili tu kufanya uchaguzi. Hivyo sioni kama viongozi wetu wa siasa wanazingatia suala hili nyeti,” anasema.
Kwa sasa kampeni inaendelea. Lakini itashika kasi wakati wabunge watakapopitisha muswada wa watoto kuwa sheŕia na kuitekeleza. (END/2005)