{"id":3974,"date":"2013-01-03T13:40:01","date_gmt":"2013-01-03T13:40:01","guid":{"rendered":"http:\/\/ipsnews.net\/swahili\/2013\/01\/03\/malengo-ya-maendeleo-yategemea-vitamini-2\/"},"modified":"2013-01-03T13:40:01","modified_gmt":"2013-01-03T13:40:01","slug":"malengo-ya-maendeleo-yategemea-vitamini-2","status":"publish","type":"post","link":"http:\/\/ipsnews.net\/swahili\/2013\/01\/03\/malengo-ya-maendeleo-yategemea-vitamini-2\/","title":{"rendered":"Malengo ya Maendeleo Yategemea Vitamini"},"content":{"rendered":"<p>BRUSSELS, Janua&#341;i 3 (IPS) &ndash; Milioni mia moja na tisini &ndash; ni diadi ya wakazi katika nchi za Uje&#341;umani, Ufa&#341;ansa na nchi ya Poland wakichanganywa kwa pamoja. Hii pia ni idadi ya watoto walioathi&#341;ika na uhaba wa vitamini &#8220;A&#8221; duniani kote. Upungufu wa vitamini &#8220;A&#8221; ambayo inapatikana katika vyakula kama vile maini, ka&#341;oti &ndash; kunaweza kusababisha vifo na kusababisha upofu kwa watoto kati ya 250,000 hadi 500,000 kwa mwaka.\n<\/p>\n<p><!&ndash;&ndash;mo&#341;e&ndash;&ndash;><\/p>\n<p>Miaka mia moja baada ya mwanasayansi wa Poland Casimi&#341; Funk kuainisha dhana ya vitamini, kumekuwepo na mafanikio makubwa katika kukuza uelewa kuwa lishe sahihi ni muhimu kwa afya.<\/p>\n<p>Hata hivyo, bado kuna kazi kubwa kufanyika, hasa katika nchi zinazoendelea, kueneza elimu ya ufahamu kuwa kutatua tatizo la njaa siyo suala la kukabiliana na tatizo la lishe. Kwa sasa, asilimia 7.3 ya mzigo wa afya ulimwenguni unasababishwa na uhaba wa vitamini na lishe.<\/p>\n<p>Umaskini ni sababu kuu ya uhaba wa vitamini, hasa vitamini &#8220;A&#8221;. Mataifa mengi ya Asia ya Kusini na Af&#341;ika Kusini mwa Jangwa la Saha&#341;a yameathi&#341;ika vibaya na uhaba wa vitamini &#8220;A&#8221; &ndash; kwani watu wengi katika nchi hizi wanakula mlo unaohusisha vyakula vikuu tu vya wanga. Kwa mfano, wali unaweza kuwakilisha hadi asilimia 70 ya chakula kinacholiwa na wengi katika nchi za Asia, wakati mihogo &ndash; ambayo inaongeza wanga kwa vingi lakini haina lishe nyingi &ndash; ni chakula kikuu kwa Waaf&#341;ika walio wengi.<\/p>\n<p>Ikilinganishwa na nchi nyingi za Asia ya Kusini kama vile Bangladesh na Nepal, India imekuwa na maendeleo duni katika kuhamasisha matumizi ya vitamini &#8220;A&#8221;. Matokeo yake, India inawakilisha asilimia 37 ya waathi&#341;ika, ikiwa ni sawa na watoto milioni 80. <\/p>\n<p>Dk. Klaus K&#341;aeme&#341; wa &#8220;Sight and Life&#8221;, shi&#341;ika la Uswis linalotetea matumizi ya lishe bo&#341;a, alilaumu India kwa kutokuzingatia suala hili. &#8220;Shi&#341;ika la Afya Ulimwenguni linapendekeza kutolewa kwa dozi mbili hadi tatu za matone ya vitamini &#8220;A&#8221; kwa mwaka kwa watoto wa chini ya um&#341;i wa miaka mitano. Hii inatokana na ushahidi wa kisayansi unaoonyesha kuwa inapunguza vifo kwa asilimia 24.<\/p>\n<p>&#8220;Ni janga kuona kuwa India iko nyuma katika kutekeleza mwongozo huu, na hivyo kusababisha vifo visivyokuwa vya lazima kwa watoto,&#8221; alisema.<\/p>\n<p>Dk. Shilpa Vinod Bhatte, mtaalam wa tiba mjini Mumbai, aliiambia IPS kuwa tatizo la India kwa sehemu linasababishwa na mlo unaoliwa na wazawa: &#8220;Njaa iliyofichika na upungufu wa vitamin &#8220;A&#8221; nchini India hakutokani tu na umaskini lakini kukosekana kwa maa&#341;ifa kuhusu chakula chenye lishe bo&#341;a ambacho kinapaswa kuliwa kwa ajili ya afya bo&#341;a &ndash; vyakula vingi vinavyoliwa na watoto chini ya miaka mitano vinakuwa vya mahindi, mchele au uji wa ngano.&#8221;<\/p>\n<p>Hata hivyo, kuna dalili kuwa hali inaanza kubadilika, hasa kutokana na msukumo mpya unaofanywa na wadau wa maendeleo duniani kote kukabiliana na tatizo.<\/p>\n<p>Katika kongamano la wataalam lijulikanalo kama &#8220;Copenhagen Consensus 2012&#8221; ambalo lilikusanya wataalam waandamizi wa masuala ya uchumi duniani lilitathmini njia zenye ufanisi zaidi za kutenga pesa kukabiliana na changamoto kubwa zaidi ulimwenguni, na kutoa taa&#341;ifa kuwa &#8220;mi&#341;adi ya kuongeza matumizi ya vyakula vyenye lishe bo&#341;a ipewe kipaumble kwa wawekezaji katika afya na maendeleo duniani.<\/p>\n<p>Mmoja wa washi&#341;iki ambaye ni mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, mwanauchumi Ve&#341;non Smith, alielezea, &#8220;Moja ya vitega uchumi muhimu zaidi ni kufikisha lishe bo&#341;a kwa watu wenye lishe duni duniani. Faida za kufanya hivyo &ndash; katika suala zima la kubo&#341;esha afya, idadi ya watoto wanaokwenda shule na uzalishaji &ndash; ni kubwa mno.&#8221;<\/p>\n<p>Makadi&#341;io ya faida ya kufanya hivyo yaliyowekwa na jopo la wataalam katika &#8220;Copenhagen Consensus&#8221; ni ma&#341;a 17 katika kila dola inayotumika.<\/p>\n<p>Kufikia Malengo ya Milenia <\/p>\n<p>Wataalam wanasema kuwa faida hizi zinapaswa kuonekana katika Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs), ambayo yalikubaliwa na nchi wanachama wote wa Umoja wa Mataifa mwaka 2000 ili kukabiliana na umaskini uliokithi&#341;i na kubo&#341;esha maisha.<\/p>\n<p>Ripoti ya mafanikio ya hivi ka&#341;ibuni ya Umoja wa Mataifa ilionyesha kuwa shabaha ya kupunguza njaa na kubo&#341;esha lishe bado iko chini mno kufikiwa.<\/p>\n<p>Hasa ikiangaliwa Af&#341;ika Kusini mwa Jangwa la Saha&#341;a inakabiliwa na kiwango kikubwa mno cha njaa &ndash; nchini Bu&#341;undi, Jamhu&#341;i ya Kidemok&#341;asia ya Kongo na E&#341;it&#341;ea, zaidi ya asilimia 60 ya wakazi wana lishe duni&#8221;.<\/p>\n<p>Umoja wa Mataifa na se&#341;ikali za kitaifa hutoa matone ya vitamini &#8220;A&#8221; sawa na mahitaji ya watoto milioni 390 kati ya watoto milioni 540 wenye upungufu wa vitamini hizo, lakini kukosekana kwa u&#341;atibu kumewaacha mamilioni nje ya jitihada hizi.<\/p>\n<p>Kwa sasa, sekta binafsi imeingilia kati katika kuziba pengo, na hivyo inatoa vitamini &#8220;A&#8221; na kusaidia kujenga uwezo.<\/p>\n<p>DSM &ndash; shi&#341;ika linaloongoza kwa kuhamasisha matumizi ya vitamini duniani lenye makao yake nchini Uholanzi &ndash; limeungana na mashi&#341;ika kama Shi&#341;ika la Chakula Ulimwenguni (WFP), Benki ya Dunia, na &#8220;Muungano wa Kidunia wa Kubo&#341;esha Lishe &ndash; &#8220;Global Alliance fo&#341; Imp&#341;oved Nut&#341;ition&#8221; (GAIN), ikiwa ni pamoja na mashi&#341;ika ya misaada kama vile &#8220;Vitamin Angels&#8221;, kutoa vitamini na lishe kwa jamii maskini.<\/p>\n<p>DSM ilitoa msaada wa kifedha wa moja kwa moja &ndash; dola milioni moja mwaka 2012 kwa ajili ya kuongeza madini ya lishe katika mchele &ndash; ikiwa ni pamoja na matone ya vitamini, unga, utaalam wa kiufundi na &#341;asilimali za vifaa.<\/p>\n<p>&#8220;Vitamin Angels inasaidia zaidi ya NGOs 100 katika majimbo ya India yenye matatizo makubwa na kutusaidia kufikia ka&#341;ibu watoto milioni tatu chini ya um&#341;i wa miaka mitano ambao wako hata&#341;ini kuwa vipofu au kufa&#341;iki dunia kutokana na upungufu wa vitamini A&#8221;,&#8221; alielezea Bhatte.<\/p>\n<p>&#8220;Vitamin Angels&#8221;, pamoja na shi&#341;ika la &#8220;Sight and Life&#8221; na DSM, pia wanafanya kazi na jamii nchini India kushi&#341;ikisha wadau kutoka katika jamii, NGOs na se&#341;ikali za mitaa na viongozi wa jamii, kuanzisha malengo ya muda m&#341;efu kama vile kufanya kazi kupitia taasisi za ndani kuanzisha mfumo endelevu wa usambazaji wa vitamini A.<\/p>\n<p>Taya&#341;i kuna matokeo yanayoonekana. Michango ya sekta binafsi inaweza kuongeza idadi ya watoto wanaopata matone ya Vitamin A kufikia milioni 50 mwishoni mwa mwaka 2013. Jitihada hizi za pamoja kwa sasa zinafikia wastani wa asilimia 17 ya mahitaji ya dunia ambayo hayajafikiwa.<\/p>\n<p>Jitihada za sekta binafsi zimesababisha Umoja wa Ulaya na mataifa yake wanachama kuliangalia tatizo hilo kama muhimu katika maendeleo. Katika mkutano wa hivi ka&#341;ibuni kuhusu maendeleo, F&#341;ancesca Mosca wa Tume ya Ulaya alielezea, &#8220;Ni suala lisilovumilika kuwa watoto wengi wanafa&#341;iki dunia kutokana na utapiamlo. Muda wa kuchukua hatua ni jana, na wala siyo leo.&#8221;<\/p>\n<p>Mosca alielezea kuwa baadhi ya jitihada zimeshaanzishwa na zinazaa matunda, kwa kujikita katika mfumo wenye mafanikio wa ushi&#341;ikiano wa sekta binafsi na zile za umma. &#8220;Tumeshi&#341;iki kikamilifu katika ha&#341;akati za kuongeza lishe (SUN)&#8221;, mpango unaoongozwa na nchi ambao ulizinduliwa mwaka 2010 kuongeza ufanisi katika mipango iliyopo. &#8220;Nadhani ni kwa ma&#341;a ya kwanza kwa washi&#341;ika wote kuja pamoja: sekta binafsi, sekta za umma, wahisani na nchi washi&#341;ika.&#8221; Paulus Ve&#341;schu&#341;en, Mjumbe Maalum wa Se&#341;ikali ya Uholanzi anayeshughulikia usalama wa chakula na lishe katika maendeleo, akizungumza katika tukio hilo, alisisitiza, &#8220;Kipindi cha maisha ya mtoto wakati ambapo tunaweza kuchukua hatu ni kifupi mno. Mustakabali wa baadaye wa watoto unategemea lishe&#8230; ni kipindi ambacho hatupaswi kabisa kushindwa kuchukua hatua.&#8221;<\/p>\n<p>Lishe inahusika ka&#341;ibu katika kufikia malengo yote ya milenia &ndash; ina faida katika afya ya mtoto, kwa mfano, inaweza kuongeza idadi ya watoto wanaokwenda shule, kukuza usawa wa kijinsia kwa kuwapatia uwezo wanawake kuwa na jukumu kubwa katika afya za watoto wao, na pia kubo&#341;esha afya ya uzazi, na hivyo kupunguza kiwango cha vifo vya uzazi. <\/p>\n","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>BRUSSELS, Janua&#341;i 3 (IPS) &ndash; Milioni mia moja na tisini &ndash; ni diadi ya wakazi katika nchi za Uje&#341;umani, Ufa&#341;ansa na nchi ya Poland wakichanganywa kwa pamoja. Hii pia ni idadi ya watoto walioathi&#341;ika na uhaba wa vitamini &#8220;A&#8221; duniani kote. Upungufu wa vitamini &#8220;A&#8221; ambayo inapatikana katika vyakula kama vile maini, ka&#341;oti &ndash; kunaweza&#8230;<\/p>\n","protected":false},"author":961,"featured_media":0,"comment_status":"open","ping_status":"open","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"footnotes":""},"categories":[1],"tags":[],"class_list":["post-3974","post","type-post","status-publish","format-standard","hentry","category-headlines"],"_links":{"self":[{"href":"http:\/\/ipsnews.net\/swahili\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/3974","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"http:\/\/ipsnews.net\/swahili\/wp-json\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"http:\/\/ipsnews.net\/swahili\/wp-json\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"http:\/\/ipsnews.net\/swahili\/wp-json\/wp\/v2\/users\/961"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"http:\/\/ipsnews.net\/swahili\/wp-json\/wp\/v2\/comments?post=3974"}],"version-history":[{"count":0,"href":"http:\/\/ipsnews.net\/swahili\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/3974\/revisions"}],"wp:attachment":[{"href":"http:\/\/ipsnews.net\/swahili\/wp-json\/wp\/v2\/media?parent=3974"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"http:\/\/ipsnews.net\/swahili\/wp-json\/wp\/v2\/categories?post=3974"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"http:\/\/ipsnews.net\/swahili\/wp-json\/wp\/v2\/tags?post=3974"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}